• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MWENGE WA UHURU WARIDHISHWA NA UJENZI WA KITUO CHA AFYA NYAMAZUGO SENGEREMA

Posted on: October 7th, 2024

MWENGE WA UHURU WARIDHISHWA NA UJENZI WA KITUO CHA AFYA NYAMAZUGO SENGEREMA


Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Ndg. Godfrey Eliakim Mnzava ameridhishwa na kuweka jiwe la msingi kwenye ujenzi wa Kituo cha Afya Nyamazugo wilayani Sengerema kinachotekelezwa kwa thamani ya Tshs. Milioni 500.

Akizungumza na wananchi baada ya kuweka jiwe la msingi leo Oktoba 07, 2024 kiongozi huyo amewapongeza viongozi wa Halmashauri hiyo kwa usimamizi mzuri uliozaa mradi wenye ubora ukilinganisha na thamani ya fedha iliyotumika.

Ndugu Mnzava amesema Mhe. Rais ameamua kutoa fedha hizo kuwajengea wananchi wake zaidi ya 45,416 kutoka kwenye kata tatu za Nyamizeze, Kasenyi na Nyamazugo na maeneo ya jirani ili jamii iwe na uhakika wa kupata matibabu.

"Sengerema mmeitendea haki fedha iliyoletwa kwa ajili ya ujenzi huu, Mhe. Rais ameleta fedha hizi ili kuboresha huduma za afya, naomba muendelee kukamilisha ili kufika mwezi Disemba huduma zianze kutolewa." Amesema ndugu Mnzava.

Ujenzi wa kituo hicho cha afya uliibuliwa na wananchi wenyewe baada ya kuona wanapata adha ya kutembea umbali mrefu kufuata huduma za afya na kwa awamu ya kwanza yanajengwa majengo ya wagonjwa wa nje, kufulia, maabara na wodi ya wazazi ya kisasa.

Aidha, Mwenge wa Uhuru umezindua mradi wa maji ya bomba katika kijiji cha Chifunfu wenye thamani ya Bilioni 2.9 fedha kutoka mpango wa maendeleo ya Maji (WSDP) uliotekelezwa na mkandarasi Emirate Builders Co. Ltd ambapo kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru amewaagiza RUWASA kuongea vituo vya kutekea maji ili wananchi wote 31,423 katika vijiji vya Chifunfu, Lukumbi na Nyakahako wapate maji.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.