• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MWENGE WA UHURU WAZINDUA MADARASA 10 NG'HAYA SEKONDARI - MAGU

Posted on: July 20th, 2023

MWENGE WA UHURU WAZINDUA MADARASA 10 NG'HAYA SEKONDARI - MAGU


Leo alhamisi tarehe 20, 2023 Mwenge wa Uhuru umezindua vyumba kumi kumi (10) vya madarasa vilivyojengwa kwa shilingi milioni 200 kutoka Serikali kuu kwenye Shule ya Sekondari Ng'haya.

Akizungumza kwenye Uzinduzi huo, Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Ndugu Abdalla Shaibu Kaim ameipongeza Serikali kwa kuwajali wanafunzi na kuamua kuwajengea miundombinu hiyo ambayo itasaidia kupunguza msongamano darasani.

Ndugu Kaim amesema kutokana na miradi kadhaa iliyobainishwa shuleni hapo kama upandaji wa miti, utoaji wa elimu ya Lishe na mradi wa kuhifadhi mazingira kuhimili mabadiliko ya tabia nchi imeonesha dhamira ya dhati ya kuhakikisha wanafunzi wanajengwa kuwa wazalendo.

Akizungumza baada ya kuweka jiwe la msingi kwenye ujenzi wa wodi ya wazazi, wanaume, Stoo ya dawa na njia ya kutembea wagonjwa vilivyogharimu Shilingi milioni 750 Ndugu Kaim amewapongeza kwa usimamizi ambao utasaidia kupunguza msongamano wa wagonjwa hususani kwa wanaume kutoka 20 sasa hadi 100 pamoja na upandaji wa Miti ya matunda kuzunguka Hospitali hiyo.

"Mhe Rais ameonesha upendo mkubwa kwa makundi mbalimbali yakiwemo ya watu wenye ulemavu na anahakikisha wanapata mikopo kutoka fungu la 10% ya mapato ya ndani ili kuwawezesha kiuchumi, nawapongeza vijana kwa uzalendo kwani wamemaliza hadi marejesho" Ndugu Kaim wakati akizindua mradi wa vijana wafuga kondoo wenye thamani ya milioni 19 katika Kijiji cha Chandulu.

Katika wakati mwingine, Mwenge wa uhuru umeweka jiwe la msingi kwenye mradi wa ujenzi wa barabara ya RC Hostel yenye urefu wa KM 0.38 kwa thamani ya milioni 499 ambapo Ndugu Kaim ameagiza wakala wa barabara za mijini na vijijini (TARURA) kukamilisha kwa wakati mradi huo ili wananchi wapate huduma.

Kaulimbiu ya mbio za Mwenge wa Uhuru 2023 inasema "Tunza Mazingira, Okoa vyanzo vya Maji kwa Ustawi wa viumbe hai kwa Uchumi wa Taifa."

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.