• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

N.C.U JENGENI NIDHAMU YA MATUMIZI YA FEDHA MLIZO REJESHEWA NA SERIKALI: RC MTANDA

Posted on: April 8th, 2024

N.C.U JENGENI NIDHAMU YA MATUMIZI YA FEDHA MLIZO REJESHEWA NA SERIKALI: RC MTANDA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo Aprili 8, 2024 amewakabidhi rasmi uongozi wa chama cha Ushirika Nyanza akaunti yao Maalum maarufu kama ESCROW iliyo na zaidi ya shs bilioni 1 na kuwataka kufanya matumizi sahihi na yenye tija ya kuendeleza chama hicho.

Akizungumza katika hafla fupi iliyofanyika kwenye ukumbi wa Ofisi ya mkuu wa Mkoa, Mtanda amesema Serikali imekuwa na nia njema tangu ilipozuia matumizi ya fedha hizo mwaka 2018 na sasa baada ya kukamilika kwa mifumo ya usimamizi imezirejesha.

"Naomba niwe mkweli katika hili sitasita kuchukua hatua kali nitakapo baini kuna ubabaishaji wa matumizi ya fedha hizi,ni lazima kuwepo na mpango kazi wa matumizi yanayo lenga kukiinua chama hiki kikongwe",mkuu wa mkoa.

Amesema Serikali ya Rais Samia ina maono ya N.C.U inazidi kuwa chombo madhubuti cha kiuchumi hasa kutokana na wingi wa mali zake vikiwemo viwanda.

Naibu Mrajisi wa vyama vya Ushirika nchini Bw. Collins Nyakunga ameishukuru Serikali kwa kuitikia ombi la kurejeshewa akaunti hiyo na kuonesha imani kwa uongozi wa Nyanza kuja na mikakati madhubuti yenye kuleta mageuzi chanya ya kiuchumi.

"Mhe.mkuu wa mkoa Ofisi ya Mrajisi wa vyama vya Ushirika itaendelea kuwa karibu na N.C.U kuhakikisha kunakuwa na usahihi wa matumizi ya fedha hizi na tutasaidia kuwepo na ubunifu wa mipango ya kiuchumi,"Naibu Mrajisi

Mwenyekiti wa bodi ya chama cha Ushirika Nyanza,Benjamini Mikomangwa baada ya mali zote zilizouzwa kinyume na utaratibu kurejeshewa,ni wajibu wao sasa kuweka mipango yenye tija kwa chama hicho.

Tangu Serikali kuzuia matumizi ya akaunti ya chama hicho mwaka 2018 kwa muda wote huo ilikuwa chini ya usimamizi wa Ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mwanza.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.