• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

NDC WAHITIMISHA ZIARA YA MAFUNZO MWANZA

Posted on: January 23rd, 2026

Washiriki wa chuo cha taifa cha ulinzi leo Januari 23, 2026 wamehitimisha ziara ya mafunzo ya siku tano Mkoani Mwanza waliyoifanya katika maeneo mbalimbali mathalani kwenye miradi ya maendeleo ambayo wameitembelea kuona namna gani inatekelezwa.

Akizungumza kwenye hafla ya majumuisho Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ameishukuru timu hiyo kwa ziara yenye tija ndani ya Mkoa na amewaahidi kufanyia kazi ushauri walioutoa katika kuboresha huduma.

Akizungumzia eneo la mipango miji, Mhe. Mtanda amebainisha mipango ya serikali ya kuwajengea wajasiriamali miundombinu rafiki ya kufanyia biashara ili wawe kwenye mazingira nadhifu na yenye tija kwao.

“Tutawasiliana na wizara ya Maliasili na Utaliii kuona namna ya kushirikiana nao kwenye kuongeza elimu kwa umma juu ya kutangaza vivutio vya utalii na kuweka mikakati ya kushirikiana na wadau kukuza sekta hiyo.” Mhe. Mtanda.

Naye, kiongozi wa timu hiyo Brigedia Jenerali Matunda amesema ziara yao imezaa matunda kwani wamepata walichokikusudia na wamejifunza mbinu, teknolojia na utekelezaji wa miradi kwa ujumla jinsi bavyo serikali inafanikisha.

Amesema, wamejionea kwa macho jinsi ambavyo serikali ya Tanzania imewekeza fedha nyingi kwenye miradi katika sekta za miundombinu, kilimo, utalii, uvuvi, ufugaji na viwanda jambo linaloipa nchi uhakika wa mazao na uzalishaji na kupelekea uhakika wa usalama wa chakula kwa wananchi wake.

Aidha, wameipongeza serikali kwa kuwajengea uwezo vijana kutumia mbinu za kisasa hususani kwenye ufugaji wa kisasa wa kuku na teknolojia ya ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba unaofanywa na makundi ya vijana ambao unasaidia kuhifadhi mazingira na kulinda mazalia ya samaki katika ziwa Victoria.

Pamoja na kupongeza kwenye uimarishaji wa usafiri katika ziwa kwa kujenga kituo cha uokozi na meli ya kisasa, wanafunzi hao wa vitendo wamebainisha changamoto kadhaa ikiwemo ukatishaji wa safari za ndege ambao wamehimiza kurekebishwa ili kutoikosesha serikali fedha kutokana na kodi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MTAKUWAA MWANZA YAWEZESHA KUPUNGUZA WATOTO WA MTAANI KWA 50%

    January 26, 2026
  • RC MTANDA: DHAMIRA NI MSINGI WA KUFANIKISHA SHUGHULI ZA MWENGE WA UHURU 2026

    January 26, 2026
  • NDC WAHITIMISHA ZIARA YA MAFUNZO MWANZA

    January 23, 2026
  • WAZIRI MKUU AZINDUA MELI MPYA YA MV NEW MWANZA, ATOA MAAGIZO KWA MIRADI ILIYOSIMAMA

    January 23, 2026
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.