• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Ndege ya BOENG 787-800 DREAMLINER kupokelewa Mwanza

Posted on: July 26th, 2018


Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mhe.John Mongella ameongea na wanahabari kuutarifu umma wa wananchi wa Mkoa wa Mwanza kuhusu mapokezi ya Ndege Mpya na ya kisasa ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) aina ya “Boeing 787 – 800” Mkoani Mwanza Siku ya jumapili, saa 1:00 Asubuhi, tarehe 29 Julai, 2018.

 Amefafanua kuhusu mambo yafuatayo kuhusiana na mapokezi ya ndege hiyo kubwa na ya kisasa:-

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Uongozi wa Mhe. Dkt John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika jitihada za kuboresha huduma za usafiri wa Anga na kuliimarisha Shirika la Ndege la Taifa (ATCL) ili kuinua uchumi wa Nchi yetu, Serikali imenunua Ndege mpya na ya kisasa aina ya “Boeing 787 – 800 Dreamliner”.

Ndege hiyo ikiwa kwenye safari yake ya kwanza Mkoani Mwanza aina ya “Boeing 787 – 800 Dreamliner” itapokelewa rasmi katika Uwanja wa Ndege wa Mwanza siku ya Jumapili tarehe 29 Julai, 2018 saa 1:00 Asubuhi.


Shirika la Ndege la Taifa (ATCL) kupitia ndege zake za “Boeing 787 – 800 Dreamliner” na  “Bombadier Dash 8 – Q400” inafanya safari zake katika uwanja wa ndege wa Mwanza mara nne kwa siku kama ifuatavyo:-


Mwanza – Dar es salaam kupitia Kilimanjaro (Saa 3:20 Asubuhi – 5:40 Asubuhi – Dreamliner).

Mwanza – Bukoba (Saa 5:15 Asubuhi – 5:45 Asubuhi - Bombadier).

Mwanza – Dar es Salaam (Saa 7:15 Mchana – 9:00 Alasiri – Bombadier).

Mwanza – Dar es Salaam (Saa 2:20 Usiku – 3:40 Usiku – Dreamliner).

Amewajulisha wanahabari kuwa ndege hiyo “Boeing 787 – 800 Dreamliner” inayotegemewa kuwasili katika uwanja wa ndege wa Mwanza tarehe 29 Julai, 2018 ina uwezo wa kubeba abiria 262 (Daraja la kawaida “Economy” abiria 240 na Daraja la Biashara “Business” abiria 22).  

Hadi sasa katika ndege hiyo itakayowasili siku Jumapili ya tarehe 29 Julai, 2018, tiketi 244 zimenunuliwa kwa safari ya ndege ya asubuhi na tiketi 158 zimenunuliwa kwa safari ya ndege ya usiku, hivyo natoa wito kwa wananchi wote kuchangamkia fursa kwa kuwahi kununua tiketi chache zilizobaki.

Mkuu wa Mkoa Amewaomba wananchi wote wa mkoa wa Mwanza na maeneo  jirani tunawaomba wajitokeze kuja katika Uwanja wa Ndege wa Mwanza kushuhudia Mapokezi ya Ndege hiyo Mpya na ya kisasa aina ya “Boeing 787 – 800 Dreamliner”. Pia,amewaomba wananchi wote kuendelea kutumia usafiri wa ndege wa Shirika la Ndege la Taifa (ATCL) kwa ajili ya kuinua uchumi wetu na maendeleo ya Taifa letu.  


Mwanza: Kazi na Maendeleo

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.