• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

ONGEZENI BIDII DIMBANI ILI TUSHINDE MICHEZO MITATU ILIYOBAKI, EPUKENI HUJUMA: RC MTANDA

Posted on: April 12th, 2024

ONGEZENI BIDII DIMBANI ILI TUSHINDE MICHEZO MITATU ILIYOBAKI, EPUKENI HUJUMA: RC MTANDA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo amejumuika kwenye mazoezi ya timu ya Pamba Jiji FC kwenye uwanja mkongwe wa Nyamagana na kuwataka kukaza buti michezo yote mitatu iliyobaki ya ligi ya Championship na kuonya kusiwepo na aina yoyote ya usaliti kwa timu.

Mkuu huyo wa Mkoa aliyetinga uwanjani na kupasha mazoezi amesema michezo iliyobaki waipe uzito na kutoka na ushindi wa kishindo hasa kutokana na kupishana pointi chache na wanaonyemelea nafasi ya kupanda.

"Nawaahidi motisha zote zipo palepale alipoishia mtangulizi wangu mimi napaendeleza nimezungumza na uongozi wenu hivyo wajibu uliopo mbele yetu ni kushinda tu tukianzia mchezo wa kesho dhidi ya PGA Talent", RC Mtanda.

Aidha, Mtanda amewaonya wachezaji hao wasithubutu kujiingiza katika mchezo mchafu wa kuihujumu timu na atakayebainika hatosita kumchukulia hatua.

"Ni lazima mtambue tupo katika nafasi nzuri ya kupanda ligi kuu na pia mjihadhari na fitna zinazoweza kujitokeza ili tukwame katika malengo yetu," amesisitiza Mkuu huyo wa Mkoa aliyechezea timu ya Bunge.

Kocha Mkuu wa Pamba Jiji FC Mbwana Makatta amesema hana shaka na kikosi chake na kasoro zote za kiufundi zilizojitokeza wamezifanyia kazi.

"Mhe. Mkuu wa mkoa tumefarijika sana kuwa nawe na hasa kujumuika nasi katika mazoezi tumejiona ni mwenzetu haswa, sisi maelekezo yako yote tunayafanyia kazi ili tutimize ndoto ya kupanda ligi kuu msimu ujao,"Makatta

Mhe. Mtanda pia alitoa nafasi kwa mchezaji wa zamani wa timu hiyo Fumo Felician kutoa nasaha kwa wachezaji hao ambaye aliwakumbusha kutambua matarajio ya wana Mwanza ya kupata burudani ya ligi kuu kwa timu yao ya nyumbani waliyoikosa kwa miaka mingi.

Pamba Jiji FC maarufu kama TP Lindanda wakiwa na pointi 58 nafasi ya pili, watashuka dimbani Nyamagana Jumamosi hii kumenyana na PGA Talent kutoka Ruvuma kabla ya kufunga safari mkoani Arusha kuhitimisha michezo miwili na TMA Aprili 21 na siku saba baadaye dhidi ya Mbuni FC.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.