• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Rais Magufuli apongeza Mafanikio Hospitali ya Bugando

Posted on: July 15th, 2019


Rais.Dkt. John Magufuli amezindua miradi saba katika Hospitali ya Kanda ya Bugando ya jijini Mwanza yenye thamani ya Sh bilioni 15 huku akimwagiza Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu kuanza kufuatilia  na kuthibisha uhalali kama viongozi wote waliokwenda kutibiwa nchini India walikuwa wanaumwa au la.

Mhe.Dkt. Magufuli ametoa agizo hilo  jijini Mwanza wakati azikindua  miradi saba katika Hospitali ya Kanda ya Bugando.

“Hii  nchi ni tajiri sana isipokuwa ilikuwa inaliwa na mafisadi na mimi nimejitoa uhai wangu kwa ajili ya kupambana nao, wengine walikuwa wanakwenda India hata kutibiwa mafua, haitoshi walikuwa wanaambatana na wake zao au waume zao, nao wakifika huko anaulizwa kama aingizwe kwenye malipo.

“Yaani Mgonjwa na msindikizaji wote wanaingizwa katika malipo na gharama zote hizo zilikuwa zinaletwa Tanzania ilipe, nasema Waziri kafuatilie huko kama utakuta wengine hawakupata kibali cha kutibiwa huko, fedha hizo watalipa wenyewe na  hazitalipwa na Serikali, nimesema na wanaosikia wasikie na wasiosikia na wasisikie,”alisema.

Katika hatua nyingine Rais Magufuli ameitaka Wizara ya afya kufanya utafiti sababu ya watanzania asilimia zaidi ya 50 wanaugua saratani na moyo  huku akielekeza hatua zichukuliwe  haraka.Alisema  inawezekana wananchi hao wanapatwa na maradhi hayo kutokana shughuli mbalimbali za uchimbaji wa madini unaofanyika  na kutiririsha  sumu kwenye maji.

Pia amewataka wakurugenzi wa Jiji la Mwanza na Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela kutenga Sh. bilioni 4 kwa ajili ya kujenga jengo la abiria katika Uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa Mwanza  kwa kutumia force account huku akimtaka Mkuu wa Mkoa Mhe. John Mongella kusimamia hilo.

Katika hatua nyingine, Mhe.Rais Magufuli  ametoa ahadi ya Sh.milioni 100 kwa ajili ya ujenzi wa bweni la wasichana  na bwalo katika Shule ya Sekondari ya Mwanza. Ahadi hiyo ameitoa wakati aliposimama eneo la shule hiyo na kuongea na wanafunzi hao.

Vile vile amesema ujenzi wa daraja la Busisi linalounganisha Wilaya ya Misungwi na Sengerema lenye urefu wa kilomita 3.2 litaanza kujengwa hivi karibuni ili kuwaondolea adha wananchi ambao wanataka kuvuka.

Naye Profesa Abel  Makubi Mkurugenzi wa Hospitali ya kanda ya  Bugando akizungumza katika hafla ya uzinduzi huo,amesema  kwa  kipindi cha miaka minne wamefanikiwa kuboresha huduma za afya na kukamilisha miradi saba ambayo ni  kitengo cha  saratani, mahututi, upasuaji, oksijeni na viwanda vidogo ambavyo vitakuwa vinazalisha dawa kwa ajili ya wagonjwa.

Ameongeza kuwa asilimia 70 ya wagonjwa wa saratani ambao walikuwa wanakwenda katika Hospitali ya Ocean Road jijini Dar es Salaam walikuwa wanatoka Kanda ya Ziwa, hivyo imewapunguzia gharama na usumbufu wa kusafiri kutafuta huduma hiyo.

Ameongeza kuwa hivi sasa asilimia 65 ya wagonjwa waliokuwa wanakwenda katika hospitali ya Ocean Road wanatibiwa Bugando.

Kwa upande wake Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe.Ummy Mwalimu amesema wamefanikiwa kudhibiti na kuongeza  ukusanyaji wa mapato  kwa mwezi kutoka Sh. bilioni 1.2  mwaka 2016 hadi Sh. bilioni 3.9 mwaka huu.

“Kama Serikali  tumeendelea kushirikiana na Bugando ambapo kwa mwaka tumekuwa tukitoa Sh 1.6 bilioni kwa ajili ya kuwalipa mishahara ya watumishi kila mwezi, vile vile   kila mwezi tunatoa   Sh.  bilioni moja saratani  kwa ajili ya dawa za saratani, lengo ni kuwapunguzia  gharama wananchi maana mgonjwa mmoja alikuwa akitakiwa kutoa Sh.300,000 hadi 400,000.

“Serikali  tumeendelea kutenga fedha ambapo hivi sasa tumetoa Sh bilioni  1.7 kwa ajili ya kujenga wodi ya wagonjwa, pia  katika Mkoa wa Mwanza  tunatoa dawa za Sh bilioni 7.9 mwaka huu kutoka Sh bilioni 1.2 mwaka 2016, kwa kutambua umuhimu wa huduma za afya watu wa kanda ya ziwa tunajenga  jengo la   mama na mtoto pale hospitali ya Mkoa –Sekoutoure,”alisema Mhe. Mwalimu.

Hata hivyo ameongeza kuwa Serikali imefunga  mashine   mpya za kisasa  katika vituo vya damu zenye thamani ya Sh bilioni 13.2 kwa ajili ya  maradhi ya damu lengo  likiwa ni kupata damu salama katika mikoa ya Kanda Ziwa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.