• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Rais Mkapa aishauri TCU kuhusu vyuo vikuu

Posted on: July 2nd, 2019


Rais mstaafu, Mhe.Benjamin Mkapa ameishauri  Tume ya vyuo Vikuu Tanzania (TCU)  kuvishirikisha vyuo binafsi katika  majadiliano  yoyote pale inapokusudia kufanya jambo lolote juu ya  elimu ya juu, kwani kufanya hivyo kutaondoa malalamiko  dhidi  yao na kuleta uwazi.

Ushauri huo aliutoa   jijini Mwanza  katika  uzinduzi wa maadhimisho ya  miaka 20  tangu kuanzishwa kwa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino (SAUT) ambapo Mhe. Mkapa alisema TCU ambayo  ndiyo mdhibiti mkuu wa elimu ya juu na mshauri wa serikali inapaswa kufanya kazi kwa ukaribu na vyuo binfasi.

Alisema  TCU  yapo malalamiko mengi kutoka vyuo binafsi juu ya uminywaji wa uhuru kutokana na uwepo vya sheria kadhaa  jambo ambalo linazorotesha ustawi  vya vyuo binafsi hususani vile  vichanga, hivyo alishauri  tume hiyo kuongeza ushirikishwaji kwa kila hatua ili kuijenga Tanzania yenye usawa katika elimu.

“Miaka 20 ya SAUT si  mchezo, nawapongeza sana kwa kazi mliyofanya ya kutoa elimu bora na tunashuhudia baadhi ya viongozi wa Serikali  wamepitia hapa, hapa Tanzania tunavyo vyuo  48   ambapo 15 ni binafsi hivyo binafsi naomba kushauri TCU  isiwe na sheria  za kuminya uhuru   wa vyuo binafsi.

“Washirikishwe kwa kila hatua katika mapendekezo yote maana bila vyuo binafsi hatuwezi kusema Serikali itatosheleza kwa kila kitu, niwahakikishie SAUT  fanyeni kazi yenu mkiwa kifua mbele jisikieni nyinyi ni miongoni mwa vyuo bora Tanzania kwa kuwa matunda yake yanaonekana lakini kubwa zaidi vyuo vya Serikali navyo vinapaswa kushirikiana na  binafsi,”alisema.


Hata hivyo Mhe. Mkapa aliweza kutoa pongezi kwa uongozi wa SAUT kutokana na kazi kubwa waliyofanya tangu mwaka 1998 kwa kupanua chuo hicho na kuanzisha vitivo kadhaa  ambapo kwa pamoja maendeleo yamepatikana huku akisisitiza  kwamba malengo waliyojiwekea ya miaka mitano  ijayo yatafanikiwa kwa kuwa tayari wamejenga msingi imara.


Awali Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Mhe.Profesa Costa  Mahalu  aliishukuru Serikali kwa kushirikiana katika utoaji wa elimu ya juu huku akiomba  kushirikishwa kwa baadhi ya mambo kabla ya kutoa maelekezo kwa vyuo  vikuu.


Profesa Mahalu ambaye alijikita sana kueleza historia  ya chuo hicho huku akiwataja viongozi wengi  wa Serikali  na wabunge walisoma  SAUT  akiwamo  Waziri wa Madini, Mhe. Dotto Biteko, Msemaji Mkuu wa Serikali, Dk. Hassan Abbas, Mkuu wa Mkoa wa Manyara,  Alexander Mnyeti kwamba ni matunda ya chuo hicho.


Pia aliwataja, John  Heche, Ezekiel Wenje, Moses Machali, Zamaradi Kawawa na wengine  wengi ambapo alisema huo ni mfano kwamba SAUT inawaandaa wasomi  ambao  wanaonekana  ndani ya jamii na mamlaka za uteuzi huku akisisitiza hiyo ni kutokana na mfumo unaotumika kuwaandaa kimaadili.


Profesa Mahalu alimshukuru Mkapa kwa kuwajengea lami kutoka barabara kuu ya Mwanza –Shinganya hadi chuoni hapo na kumtolea mfano kama kiongozi wa kwanza kuruhusu wanafunzi wa vyuo binafsi kupata mkopo kutoka serikalini wakati wa utawala wake.


“Kikubwa  ni kuiomba  na kuishauri Serikali na sekta binafsi  kuwatumia wasomi mbalimbali katika mipango ya maendeleo ya nchi ili wananchi waweze kufaidika na matunda ya usomi wao, hivyo  Serikali ivishirikishe vyuo binafsi katika majadiliano ya  mipango  sekta ya elimu badala ya kujifungia wenyewe,”alisema Profesa Mahalu.


Naye Makamu wa Rais wa Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC)  na Askofu wa Jimbo la Geita Mhasham Flaviana Matindi, alisema wahitimu wengi wa vyuo vikuu wanapohitimu huwa wana mawazo ya kupata ajira lakini ndani ya chuo hicho wamewajengea misingi ya kujiamini na kujiajiri.


“Miaka mitano ijayo tumejiwekea malengo ya  kutengeneza tunu, hatutaki kuwa na majengo makubwa ambayo hayaendani na ujuzi tunaoutoa ndio maana tumeagiza  kila kitivo  kwa kila mwezi ni lazima kijitathmini ili kujua mapungufu yao na kuyafanyia kazi, kwa miaka hiyo ijayo tunataka kuwa na tunu kila kitivo,”alisema.


Kwa upande wake Waziri wa madini Mhe.Doto  Biteko,alisema  ni wakati muafaka kwa watanzania kutoka katika misingi ya kulalamika na kwenda misingi ya vitendo ambapo alisisitiza kuwa  kwa  utawala wa  sasa hautoi mwanya kwa  kijana kusubiria kushikwa  mkono ili kupata ajira, kila  mmoja anatakiwa kuonyesha  uwezo wake.

Pia alisema anafarijika kuona  akiwa waziri wa madini huku akiwa na kumbukumbu ya kuwa Rais wa Serikali ya wanafunzi wa  SAUT enzi  hizo akiwa anasoma hapo ambapo alidokeza kuwa baraza lake aliloliteua,  nao pia ni viongozi wa Serikali na wabunge kwa sasa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.