• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAIS SAMIA AWEKEZA MIRADI MINGI YA MAJI NA AFYA KUWASAIDIA WANAWAKE NCHINI : RC MAKALLA

Posted on: March 8th, 2024

RAIS SAMIA AWEKEZA MIRADI MINGI YA MAJI NA AFYA KUWASAIDIA WANAWAKE NCHINI : RC MAKALLA


*Asema nchi imetulia, Rais Samia ni wa kuigwa kwa Demokrasia*


*Atoa wito kwa NGO's kuendelea kupinga ukatili wa kijinsia*


*Wanawake wakandarasi wapewe haki sawa kwenye kuteleza miradi*


*Madawati ya kupinga ukatili wa kijinsia kwenye maeneo yote yawepo*


*Maambukizi ya VVU yafikia 7.2 waathirika zaidi ni wanawake na wasichana*


*Mikopo ya Wanawake itarejea, Serikali inaandaa utaratibu*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amesema kuwa upatikanaji wa maji mkoani Mwanza utafikia asilimia 86 kutoka 70 ya sasa vijijini ifikapo mwaka 2025 kutokana na uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali kwenye miradi ikiwa ni katika kuhakikisha wanawake wanaondolewa adha hiyo.

CPA Makalla amebainisha hayo leo, Machi 08, 2024 alipokua akihutubia wanawake wa Mkoa wa Mwanza kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani yaliyofanyika kimkoa kwenye viwanja vya Amani wilayani Misungwi.

Makalla amesema Rais Samia amekua akitoa fedha nyingi kwenye miradi mathalani zaidi ya Bilioni 30 kwenye mradi wa kata ya Kolomije wilayani Kwimba ambapo anakusudia kuwatua wanawake ndoo kichwani na akabainisha kuwa mikopo kwa Wanawake itarejea na sasa Serikali inaandaa utaratibu mzuri wa kutoa.

Aidha, ametoa wito kwa wakuu wa wilaya pamoja na asasi zisizo za kiserikali kuhakikisha wanaendelea kutoa elimu ya madhara ya ukatili wa kijinsia kwa wananchi ili iwe na ufahamu na kuweza kujilinda na kuwa na ujasiri wa kuripoti waonapo madhila ya aina hiyo kwenye jamii.

Akizungumzia maambukizi ya virusi vya ukimwi yaliyofikia asilimia 7.2 amebainisha kuwa Mkoa huo unaendelea na mikakati ya kuondokana na madhila yanayopelekea maambukizi kuwa juu na akawataka wazazi kuzingatia malezi bora ya watoto kwenye kaya zao.


"Mkoa wetu una viongozi wanawake kwa ngazi mbalimbali mathalani Wakuu wa Wilaya watatu tena wanachapa kazi vizuri pia tunaye MNEC, mkurugenzi wa mamlaka ya maji ya mkoa tena amekua kinara katika kuendeleza mkakati wa kumtua mama ndoo kichwani." Makalla.



Akitoa salamu za wanawake mkoa wa Mwanza Mwenyekiti wa jamati ya maadhimisho hayo Zeyana Seif amesema ameiomba Serikali kuongeza shule za bweni kwenye shule za sekondari ili kundi hilo lipate mazingira mazuri ya kupata elimu na kupumzika badala ya kutembea umbali mrefu na kukutana na vishawishi.


"Ongezeko la watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu, matumuzi ya dawa za kulevya, mimba za utotoni, ukatili pqmoja na watoto wa mtaani ni miongoni mwa matokeo ya wanawake kujikita kwenye utafutaji na kujihusisha na shughuli za uchumi hivyo tunaiomba Serikali irejeshe nfuko wa uwezeshaji kwa wanawake." Bi. Zeyana.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake (UWT) Mkoa wa Mwanza  Mhe. Adela Mayengela ametoa wito kwa wanawake kuisherehekea siku hiyo kwa dhati huku wakijiamini lakini akawakumbusha wajibu wa kuhakikisha wanachapa kazi ili kuliletea Taifa maendeleo na kumuunga mkono Rais Samia.


Jackline Aluta kutoka Shirika la Aman Girls Foundation amesema Shirika hilo kupitia mradi wa Afya, Elimu na uhifadhi wa jamii wanahakikisha wanawalinda mabinti kuanzia rika la umri balehe ili waweze kufikia ndoto zao kwa kupata elimu na sio kuingia kwenye masuala ya ngono.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.