• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAIS SAMIA MGENI RASMI TAMASHA LA BULABO, RC MAKALLA AWAALIKA WANANCHI KUMPOKEA

Posted on: June 8th, 2023

RAIS SAMIA MGENI RASMI TAMASHA LA BULABO, RC MAKALLA AWAALIKA WANANCHI KUMPOKEA


*Rais Samia kugagua Miradi ya kimkakati*


*Awataka viongozi kujiandaa na ugeni*


*Awakumbusha wakuu wa taasisi kutoa huduma bora*


Mkuu wa Mkoa wa Kwanza Mhe. CPA. Amos Makalla amewataka Wakuu wa taasisi na wananchi kujitokeza kwa wingi kumpokea Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye atawasili Juni 12, 2023 kwa ajili ya uzinduzi wa tamasha la Bulabo pamoja na kutembelea Miradi ya kimkakati iliyopo  Mkoani Mwanza.

Mhe.CPA Makalla amesema hayo leo Juni 8, 2023 kwenye kikao kazi na Wakuu wa Taasisi zinazofanya kazi Mkoani Mwanza ambacho kimefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kikiwa na lengo la kupokea taarifa mbali mbali za miradi inayotekelezwa na taasisi hizo.

"Niwaombe Wakuu wa Taasisi pamoja  wananchi wote wa mkoa wa mwanza kujitokeza kwa wingi katika kumpokea Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye tarehe 12, Juni 2023 atawasili Mkoani hapa na tarehe 13, Juni 2023 atakwenda kwenye uzinduzi wa tamasha la Bulabo na tarehe 14, Juni 2023 atatembelea miradi ya kimkakati," Amesema  Mhe. Makalla


"Naomba kila Mkuu wa Taasisi auone ugeni huu kuwa ni ugeni wetu hivyo tunakila sababu ya kutoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa katika kutoa taarifa na ushirikiano wa hali na mali." Ameongeza Mhe. CPA Makalla.

Aidha, Mhe. Makalla ametoa rai kwa Wakuu hao wa Taasisi  kuhakikisha wanatoa huduma bora kwa wananchi ili kusaidia mkoa kuwa katika hali ya usalama.


"Niwaombe muitumie ofisi yangu vizuri katika kuhakikisha tunatoa huduma bora kwa wananchi na hali ya ulinzi na usalama inakua shwari, wote tunategemeana katika kuhakikisha tunatoa huduma bora," Ameongeza CPA Makalla.

"Mimi  Mkuu wa Mkoa ni kiongozi wa shughuli zote  katika Mkoa huu nawaomba ushirikiano katika kutimiza majukumu tuliyopewa na Mhe. Rais,"Mhe. Mkuu wa Mkoa.


Pia, Mhe.Makalla ameitaka Bodi ya Pamba ikifikia msimu ujao wa maandalizi ya kulima na kuuza pamba changamoto zote zilizo ainishwa katika uwasilishaji  zifanyiwe kazi  ili msimu utakapoanza ziwe zimekwisha.

Naye, Mhandisi Paschal Ambros Meneja wa Tanroad Mkoani Mwanza amesema miradi wa kimkakati wa ujenzi wa  daraja la JP Magufuli Lenye urefu wa kilomita 3 ukikamilika itainua maendeleo ya kijamii na kiuchumi katika Mkoa kwakuwa litaunganisha Wilaya za Misungwi na Sengerema,  ambazo zimetenganishwa na ziwa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.