• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAS Balandya awapa somo Wakandarasi Mwanza

Posted on: September 29th, 2022


Katibu Tawala Msaidizi, Seksheni ya Miundombinu Mkoa wa Mwanza, Msanifu wa Majengo Chagu Ng'homa ameonya kuwa wakandarasi ambao hawatakidhi Sifa zinazohitajika hawatapata kazi za Ujenzi wa Miradi ya Maendeleo Mkoani humo huku akiwataka watakaopata kutekeleza kwa mujibu wa mikataba yao.

Amesema hayo leo katika Kikao Kazi cha Wahandisi kutoka Sekta ya Barabara (TARURA) na Majengo kutoka kwenye Halmashauri za Mkoa huo kwa niaba ya Katibu Tawala Mkoa Balandya Elikana walichoketi kufanya tathmini ya miradi iliyotekelezwa mwaka wa fedha uliopita na itakayotekelezwa 2022/23.

"Hali ya utekelezaji wa miradi mkoani Mwanza tunajivunia maana miradi mingi imeenda vizuri na leo tumekuja kuwekeana mikakati ya kuendelea kuboresha zaidi miradi yetu kwa mwaka huu na ili tufanikishe haya ni lazima tuwe na weledi kwenye Utekelezaji wa miradi hivyo tunazingatia" Amesema Ng'homa.

Meneja wa Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA) Mkoa wa Mwanza, Mhandisi Goodluck Mbanga amesema kuwa bajeti ya kutekeleza miradi ya barabara Mkoani humo imekua ikiongezeka kila mwaka huku akibainisha kuwa kwa mwaka wa fedha  2022/23 imetengwa zaidi ya Shilingi Bilioni 25 na  kuna mikataba zaidi ya 90 itatekelezwa tofauti na 2021/22 ilipotekelezwa mikataba 43.

Bi. Maua Ally, Afisa Mahusiano na Elimu kwa Umma kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) wakati akitoa Mada ya Maadili na Changamoto za Rushwa kwenye utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo kwa niaba ya Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Mwanza amesema thamani ya fedha kwenye miradi ya ujenzi ni lazima ionekane ili wananchi wapate miradi bora itakayodumu kwa muda mrefu.

Ameongeza kwa kuwasihi wahandisi kufanya kazi kizalendo na kutojihusisha na vitendo vya Rushwa kwa namna yoyote kwani haina manufaa bali ni dhuluma na dhambi kwa mwenyezi Mungu na kwamba mtu akijihusisha nayo ataharibu kizazi chake kwani tabia hiyo inarithi kwenye vizazi hadi vizazi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.