• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAS Balandya awatangazia wastaafu watarajiwa wa mfuko wa PSSSF fursa zilizopo Mwanza

Posted on: September 13th, 2023

RAS Balandya awatangazia  wastaafu watarajiwa wa mfuko wa PSSSF fursa zilizopo Mwanza


Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Ndg. Balandya Elikana amewashauri wastaafu watarajiwa wa mfuko wa PSSSF kuchangamkia fursa zilizopo Mwanza ukiwemo mgodi wa Nyanzaga uliopo Wilayani Sengerema.

Mtendaji huyo wa  Mkoa ametoa kauli hiyo leo Jijini Mwanza kwenye ukumbi wa Rock City Mall wakati wa ufunguzi wa semina ya siku mbili ya wastaafu watarajiwa ambapo amesema mgodi huo unaotarajia kuanza kazi hivi karibuni utahitaji huduma mbalimbali hivyo ni eneo mwafaka la kujipatia kipato.

"Ndugu zangu wastaafu watarajiwa tumieni semina hii mpate kuelimika vizuri ili iwe na tija kwenu siku za baadaye,mgodi wa Nyanzaga ambao ni  pili kwa ukubwa baada ya Geita utahitaji huduma nyingi kama vyakula hivyo ukijikita kwenye ufugaji bora utaweza kusambaza mayai au nyama,"Balandya

Ameongeza kuwa rasilimali ya maji ya ziwa Victoria pia ni eneo lingine la uwekezaji kama ufugaji wa kisasa wa samaki kwa njia ya vizimba au uvuvi kwa kutumia boti za kisasa zilizotolewa na Serikali.

Ameupongeza pia mfuko wa PSSSF kwa utaratibu wa kutoa semina hiyo kwenye mikoa mbalimbali ambayo inawasaidia wastaafu hao watarajiwa kujengewa uwezo kwani baadhi yao huishia kutapeliwa au kujikuta wakifanya maamuzi yasiyo sahihi ya matumizi ya fedha zao.

"Baadhi ya wastaafu wamejikuta wakipatwa na maradhi au kuchanganyikiwa na wengine kupoteza maisha kutokana na walichotarajia kiwasaidie kimetumika ovyo na kujiweka katika hali ya umasikini,hivyo naamini kupitia jukwaa hili mtaelimika vyema na fedha zenu kuwa salama kwa muda wote wakati wa kustaafu",amesisitiza Mtendaji huyo wa Mkoa.

Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa PSSSF Bi.Vupe Ligate amebainisha lengo la semena hiyo ni kuhakikisha wateja wao wanakuwa na maamuzi sahihi ya matumizi ya fedha zao  pale wanapoamua kujishughulisha na miradi mbalimbali ya kujiongezea kipato kwa familia,ndiyo maana kwenye semina hiyo wapo wataalamu wa fani mbalimbali watakao toa elimu  pamoja na Taasisi za kifedha zenye wajibu wa kutoa mikopo na kutunza fedha hizo.

"Ndugu mgeni rasmi hapa tunao wataalamu wa ufugaji nyuki,wachumi na wengineo ambao kwa siku mbili watatoa elimu kwa wateja wetu ambayo itakuwa ni dira mwafaka kwao utakapo fika muda wa kuamua kipi cha kufanya,"Bi.Ligate.

Kauli mbiu ya semina hiyo inasema "Wekeza Mafao yako sehemu salama kwa uhakika wa Ukwasi".

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.