• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAS Mwanza aahidi kuzifanyia kazi changamoto Kituo cha Hija Nyantakubwa Sengerema

Posted on: June 12th, 2022

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Ngusa Samike ameahidi kuharakisha huduma za msingi kuwepo kwenye Kituo cha Hija Nyantakubwa kilichopo Wilayani Sengerema Mkoani Mwanza.


Katibu Tawala Ngusa amesema hayo mwishoni mwa wiki hii alipohudhuria Misa Takatifu ya Hija iliyofanyika eneo la Msalabani,amesema tayari eneo hilo limeshajengwa makazi ya Viongozi wa Dini kwa ajili ya kutoa huduma za kiroho hivyo atahakikisha mradi wa umeme unafikia eneo hilo.


"Nimesikia kuna changamoto ya upatikanaji wa mchanga mzuri wa ujenzi eneo hili, na eneo lenu mliopokuwa mnachimba kuna ujenzi wa Chuo cha Ardhi,naomba niseme tumelipokea na tutaenda kulifanyia kazi Mkoani." Katibu Tawala Mkoa.


Aidha katika salamu zake za Hija Katibu Tawala wa Mkoa Ngusa amewakumbusha Waumini kuyaishi  vyema matendo ya kumpendeza Mungu hasa wakati wa mfungo wa Kwaresima kujinyima kwa dhati na kuwajali wanaotaabika na maisha.

Askofu wa Jimbo la Geita Mhashamu Flavian Kasala amesema Hija hiyo ya siku mbili ni nafasi muhimu kwa Waumini kumrudia Mungu na kuishi kwa amani na kusameheana.


Katika Misa hiyo Takatifu  ilikwenda pamoja na zoezi la Harambee ya kuchangia ujenzi wa Kituo hicho cha Hija pamoja na nyumba ya Mapadre ,iliyoongozwa na Katibu Tawala wa Mkoa Ngusa huku Waumini wakihamasika na kutoa matoleo mbalimbali zikiwemo fedha taslimu na ahadi.


Kituo hicho cha Hija kipo eneo la Msalabani  Parokia ya Nyantakubwa chini ya Jimbo la Geita kwa mujibu wa taratibu za Kanisa Katoliki.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.