• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAS MWANZA ATOA RAI KWA WAFANYABIASHARA WADOGOWADOGO

Posted on: February 16th, 2024

RAS MWANZA ATOA RAI KWA WAFANYABIASHARA WADOGOWADOGO


*Awataka maafisa husika  kushirikiana kikamilifu na kuwajibika katika kuwahudumia wafanyabiashara wadogo wadogo.


*awataka  kufanya utambuzi na usajili na kutekeleza maagizo kwa kuzingatia mafunzo waliyopewa


Katibu Tawala wa mkoa wa Mwanza Ndg. Balandya Elikana leo Februari 16, 2024 amezindua mafunzo ya siku moja ya utambuzi, usajili na utoaji vitambulisho kwa wafanya biashara wadogowadogo mkoani Mwanza mfumo huo unaofahamika kama Wafanyabiashara wadogowadogo.

Akizungumza na maafisa Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wanawake na Makundi maalumu, maafisa biashara na maafisa Tehama pamoja na washiriki mbalimbali katika ukumbi mdogo wa Ofisi ya mkuu wa mkoa,Mtendaji huyo wa Mkoa amewataka Maafisa hao kuongeza juhudi ya uwajibikaji ili wafanyabiashara hao wapate fursa mbalimbali

Amebainisha hayo kutokana na kuwepo kwa idadi kubwa ya wafanya biashra wadogowadogo wambao hawatambuliki hivyo amewataka maafisa hao  kuwasajili pamoja na kuwapa vitambulisho wafanya biashara hao.

“Tumekuwa na idadi kubwa ya wafanyabiashara wadogowadogo na Serikali imekuwa ikitoa maelekezo mbalimbali,agenda ya Serikali ni kuhakikisha wafanya biashara wanapatiwa fursa mbalimbali na mikopo pamoja na kuwatambua na kuwapanga ili wazidi kufanya biashara zao kwa urahisi” Amesema Balandya

Hata hivyo ameongeza kueleza umuhimu wa mafunzo hayo ambayo yamelenga kuleta mageuzi mbalimbali kwa wafanyabiashara huku akiwataka maafisa jamii hao kushirikiana pamoja ili kuweza kufanikisha zoezi hilo huku akiamini juhudi zao katika  utendaji wao wa kazi

Nae Afisa maendeleo ya jamii,mkoa wa Mwanza Bi.Janeth Shishila ameeleza kuwa zoezi zima la mafunzo hayo ni kurahisisha utambuzi wa idadi ya wafanyabiashara, huku akiwahakikishia wafanyabiashara hao kuwa zoezi hilo halitakuwa na athari zozote katika jamii

“Zoezi hili linafaida kwa wamachinga wadogowadogo kwa kuanza kupata kanzi data na kufahamu walipo na shughuli wanazozifanya” Amesema bi. Janet

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.