• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAS Mwanza awaahidi JWTZ Ushirikiano kwenye Miradi Mkoani humo.

Posted on: December 29th, 2023

RAS Mwanza awaahidi JWTZ Ushirikiano kwenye Miradi Mkoani humo


Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Balandya Elikana ameliahidi Jeshi la Wananchi nchini (JWTZ) kushirikiana nao kwenye Miradi mbalimbali ya kimkakati iliyopo mkoani humo ili iimarike kiulinzi na kiusalama kwa tija ya wananchi.

Mtendaji huyo wa Mkoa amezungumza hayo mapema leo Disemba 29, 2023 Ofisini kwake wakati wa mazungumzo mafupi na Meja Generali Shaaban Mani ambaye ni mkuu wa kamandi ya anga kutoka JWTZ, amesema kutokana na Teknolojia inavyozidi kushika kasi jeshi hilo lina umuhimu mkubwa kuhusishwa kwenye miradi hiyo ili nalo lijipange vizuri katika kutekeleza majukumu yake.

"Tuliona mwaka 1978 wakati wa vita dhidi ya Idd Amin Daraja la mto Kagera lilivyo shambuliwa na adui,hilo ni somo kwetu vikosi vya jeshi kuwa karibu na miundombinu kama hiyo," amefafanua Balandya wakati akizungumza na mgeni wake.

Balandya amebainisha Mwanza ina miradi mingi inayoendelea kujengewa kuanzia Reli ya kisasa,SGR,Daraja la JP Magufuli na Meli ya abiria Mv Mwanza na kituo cha kimataifa cha ulinzi na uokoaji Ziwa Victoria kilichopo mbioni kujengwa cha Jumuiya ya Afrika Mashariki ambacho makao makuu yake yatakuwa Mwanza,miradi yote hiyo watashirikiana na Jeshi ili izidi kuwa endelevu

"Sisi kama Jeshi ni wajibu wetu kuhakikisha muda wote Taifa lipo salama,nimefika Mwanza ili kukagua miundombinu yetu iliyopo chini ya kikosi cha anga na kama kuna changamoto ni kuzifanyia kazi haraka,"Mej Gen.Mani.

Katika mazungumzo hayo Mkuu huyo wa kikosi cha anga amemuomba Katibu Tawala wa Mkoa kuwapa maeneo yaliyovamiwa na wananchi ili waweze kufanya shughuli zao kwa ufanisi zaidi.

"Maeneo ya Jeshi ni lazima yawe mbali na makazi ya wananchi,kitendo cha nyumba za raia kuwa karibu yetu ni hatari pia kwa usalama wa nchi kwa mtu atakaye kuwa na nia mbaya,"amesisitiza Mej.Gen.Mani

Wakati huo huo Ndg.Balandya Elikana amemkaribisha rasmi Mkuu mpya wa Uhamiaji Mkoa wa Mwanza,Kamishna msaidizi,Kola Kayumba anayechukua nafasi ya mtangulizi wake Kamishna msaidizi Peter Mbaku anayehamia Mkoa wa Rukwa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.