• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAS MWANZA AWATAKA VIJANA KUTUMIA MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI KUJIINUA KIUCHUMI

Posted on: October 16th, 2023

RAS MWANZA AWATAKA VIJANA KUTUMIA MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI KUJIINUA KIUCHUMI


Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Chagu Nghoma amewataka Vijana mkoani humo kutumia Takwimu za matokeo ya Sensa ya watu na Makazi ya mwezi Agosti 2022 kujikita kwenye Sekta zenye tija ili kujiimarisha na kujiinua kiuchumi.

Ametoa rai hiyo leo Oktoba 16, 2023 wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya usambazaji na matumizi ya matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi yaliyotolewa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu kwa Vijana Mkoani humo chini ya Uratibu wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

Amesema, vijana ndio kundi linalotegemewa kuchagiza uchumi wa nchi kwa sasa na siku za baadae hivyo ni lazima wawe na taarifa sahihi za eneo gani lina tija endapo watajihusisha nalo mathalani biashara, kilimo au uvuvi na kwamba majibu ya suala hilo yanapatikana kwenye takwimu zilizokusanywa wakati wa Sensa.

"Suala la ajira ndilo eneo lenye changamoto zaidi kwa vijana wa Mwanza, hivyo tunaishukuru sana Ofisi ya Taifa ya Takwimu kwa kuwapa mafunzo kundi hilo kwani wataweza kutumia takwimu hizo kuona sehemu gani ina fursa ya kujiinua kiuchumi endapo watajikita nayo." Amefafanua.

Aidha, ametumia wasaa huo kumshukuru Rais Samia kwa kuweka fedha nyingi kwenye miradi ya kuwainua vijana kiuchumi kama ujenzi wa kesho bora kwenye kilimo na mifugo (BBT) ambapo ametolea mfano shamba la Taifa la Mifugo la Mabuki ambapo vijana wamekuwa wakipatiwa mafunzo ya ufugaji wa kisasa na wakifikisha ujuzi huo kwa wengine watasaidia kuboresha sekta hiyo.

Ndugu Nghoma ametaja pia mikopo inayotolewa kwa ajili ya kufanya ufugaji wa kisasa kwa njia ya vizimba na ufadhili wa vijana kwenye mafunzo ya uanagenzi kupitia vyuo vya Ufundi stadi nchini (VETA) kuwa ni miongoni mwa maeneo yenye fursa ya kupata ujuzi na kusaidia kujikita kwenye uzalishaji wenye tija.

Mdoka Omary, Mtakwimu mwandamizi kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu amesema kuwa mafunzo hayo ni katika utekelezaji wa muongozo uliozinduliwa na Rais Samia wa kuhakikisha matokeo hayo yanasambazwa katika ngazi zote ili takwimu hizo zifike hadi vijijini.

Amefafanua kuwa matokeo ya Sensa ya watu na Makazi yanatoa majibu na fursa ya eneo gani liongezewe nguvu katika suala la utegemezi ambao imefikia 87 asilimia kwa kila watu 100 wa umri wa kufanya kazi na Mwanza imefikia zaidi ya asilimia 100 hivyo inatoa fursa kwa vijana kujikita kwenye uzalishaji ili kutoka kwenye uzalishaji.

Mkoa wa Mwanza unashika nafasi ya pili kwa idadi kubwa ya watu nchini ukitanguliwa na Mkoa wa Dar es salaam kwa kuwa na idadi ya watu Milioni 3.7 huku ikiwa na Kaya Laki Saba ambapo Jiji la Mwanza likishika nafasi ya kwanza kwa kuwa na watu Laki Tano huku Ukerewe ikiwa na watu wachache zaidi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.