• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Gabriel awapongeza Watumishi wa Ofisi yake kwa kazi nzuri

Posted on: July 1st, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Mhandisi Robert Gabriel amewapongeza na kuwashukuru watumishi wa Ofisi yake kwa ushirikiano uliozaa ufanisi mkubwa kwenye kazi kwa kipindi cha mwaka wa fedha ulioishia juni 30, 2022.

Amebainisha hayo kwa furaha mchana wa leo Julai 1, 2022 katika kikao cha kufungua Mwaka mpya wa fedha 2022/23 kilichowakutanisha watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa ili kufanya tathmini ya kazi zilizotekelezwa katika kipindi cha mwaka wa fedha uliopita.

"Hongereni kwa kazi nzuri mliyofanya mwaka ulioisha, Mwaka huu Mpya tuna deni kubwa katika kuwahudumia wananchi kupitia ofisi zetu hivyo pamoja na tathmini tunayoenda kufanya ni wajibu wetu kuongeza ushirikiano na kuombeana kheri katika kazi." Mkuu wa Mkoa.

Vilevile, amewakumbusha watumishi wa Ofisi hiyo kuzingatia Melengo ya Makusanyo yaliyo mbeleni na amewataka kuketi na wataalamu wanaohusika na makusanyo katika halmashauri zote ili kuangalia kwa pamoja ni viashiria vipi vya makusanyo vinaonesha kuleta tija.

"Kwangu mimi siwaoni nyie kama wafanyakazi wenzangu bali nawaona kama ndugu zangu, ndani ya mwaka huu tumefanya makubwa nami naongeza maombi ili tuwe na afya njema na tuzidi kuwa bora katika kazi." Mkuu wa Mkoa amesema.

"Hivi karibuni nimezunguka kwenye Halmashauri zote za Mkoa huu kwenye Vikao vya Mabaraza ya CAG na nimeona changamoto kadhaa na tunahitajika sana katika kuwasaidia hasa kuepuka matumizi mabaya ya fedha ili kuepuka hoja." Amesema, Mhe. Gabriel.

Naye, Katibu Tawala wa Mkoa Ngusa Samike amemshukuru Mhe Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuipatia Ofisi hiyo zaidi ya Tshs Bilioni 1 ambazo zinatekeleza maboresho ya Miundombinu pamoja na ujenzi wa Nyumba za Makatibu Tawala Wasaidizi, Ukarabati wa Ofisi za Wakuu wa Wilaya na Ujenzi wa Ofisi za Maafisa Tarafa.

"Ndugu watumishi wenzangu, tumekutana hapa leo kufanya tathmini ya tulikotoka na kuweka mikakati mipya kwa mwaka wa fedha tunaouanza katika kuwahudumia wananchi kwa ufanisi na kuboresha mazingira ya kazi." Amesema Samike.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.