• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA AAGIZA TANESCO NA RUWASA KUPELEKA HUDUMA ZA MAJI NA UMEME KWENYE UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI YA WASICHANA MWANZA

Posted on: July 11th, 2023

RC MAKALLA AAGIZA TANESCO NA RUWASA KUPELEKA HUDUMA ZA MAJI NA UMEME KWENYE UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI YA WASICHANA MWANZA


*Awapongeza Magu kwa Usimamizi mzuri wa Ujenzi*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla ameupongeza uongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Magu kwa Usimamizi mzuri wa Mradi na amewaagiza TANESCO na RUWASA kupeleka huduma za Umeme na Maji kwenye Shule ya Sekondari ya wasichana ya Mwanza (Mwanza Girls) inayokamilishwa kujengwa.

Mhe. Makalla ametoa agizo hilo mapema leo jumanne Julai 11, 2033 wakati alipofanya ziara kwenye kijiji cha Ihushi-Bujashi kwa ajili ya kukagua Maendeleo ya Ujenzi wa Shule Mpya ya Sekondari ya Wasichana Mwanza (Mwanza Girls) inayotekelezwa kwa zaidi ya Bilioni 3 fedha kutoka kutoka Serikali kuu.


"Mtu wa Maji na Umeme pokeeni kilichopo na utaendelea kudai fedha zingine ili wanafunzi hawa wapate maji au umeme, hizi ni huduma muhimu sana hivyo hatuwezi kuzikosa nataka muanze mpango kazi wa kutekeleza kwa haraka nawe wa barabara tengeneza kwa haraka kwa kutumia kile kidogo kilichopo." Mhe. Makalla.

"Tunamshukuru sana Mhe. Rais kwa kuweka alama hii na mabadiliko makubwa kwenye Sekta ya Elimu wilaya kwetu na Mkoa kwa ujumla, nasi tunamwombea kheri kwa Mwenyezi Mungu na tunamtia moyo aendelee kuwainua watoto wa kike wa nchi hii." amesema Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Magu, Mhe. Simon Mpandalume.


Akitoa taarifa ya Utekelezaji wa Ujenzi wa Shule ya Wasichana ya Mwanza (Mwanza Girls), Afisa Elimu Sekondari ya Magu, Beatrice Balige amesema kuwa Halmashauri hiyo imepokea Shilingi bilioni 3 kati ya nne zilizotengwa na kwamba utekelezaji kwa ujumla umefikia zaidi ya asilimia 90 na kwamba wamejiwekea mikakati madhubuti ya kukamilisha kwa wakati.

Ameongeza kuwa Halmashauri hiyo imepokea zaidi ya bilioni Moja kwa ajili ya Ujenzi wa Miundombinu mingine na kwamba Shule hiyo kwa sasa ina Changamoto ya chanzo imara cha Maji pamoja na Umeme na kutokana na ufinyu wa bajeti kwenye eneo hilo huku akibainisha kuwa shule hiyo itasaidia kuboresha mazingira ya kufundisha na kujifunzia.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.