• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA AMTAMBULISHA RASMI KOCHA MKUU WA PAMBA JIJI FC, MBWANA MAKATTA

Posted on: July 25th, 2023

RC MAKALLA AMTAMBULISHA RASMI KOCHA MKUU WA PAMBA JIJI FC, MBWANA MAKATTA


*Atambulisha jina jipya la timu kuwa ni Pamba Jiji Football Club*


*Asema timu imempata kocha mwenye viwango na uzoefu wa mechi za Ligi kuu*


*Awaomba wana Mwanza kuunganisha nguvu zao ili timu ipande Ligi kuu msimu ujao*


Hatimaye timu ya soka ya Pamba Jiji FC ya Mkoani Mwanza inayoshiriki  Ligi ya Championship imempata kocha Mkuu mpya Mbwana Makatta akisaidiana na msaidizi wake, Renatus Shija aliyeingia kandarasi ya mwaka mmoja ya kuinoa timu hiyo maarufu kama TP LINDANDA.

Akimtambulisha leo mbele ya vyombo vya Habari kwenye ukumbi mkubwa wa Ofisi yake, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.CPA Amos Makalla ambaye ni mlezi wa timu hiyo amebainisha baada ya kufanya mchakato wa kina hatimaye wamempata mtaalamu huyo wa ufundi wa uhakika.

"Namtambulisha kwenu kocha mpya Mbwana Makatta, hapa nawahakikishieni hatukubahatisha kumpata,namfahanu vyema uwezo wake na nina imani tutafika malengo yetu ya kucheza Ligi kuu msimu ujao,"CPA Makalla.

Mkuu huyo wa Mkoa ambaye ni mkereketwa wa michezo amesema baada ya kuimarisha dawati hilo la ufundi, kinachofuata sasa ni maandalizi ya timu kuingia kambini Agosti Mosi 2023 huku mtaalamu huyo wa ufundi akiendelea kuipitia ripoti ya mtangulizi wake na yeye kutoa mapendekezo yake baada ya kuwaona wachezaji uwezo wao.

"Kocha nikuondoe shaka tuna kasumba baadhi yetu kuwa na orodha ya nani umpange nani umwache katika mchezo husika,hilo la kuingiliwa hapa hutaliona na badala yake uamuzi wa mwisho utabaki kwako hata kama mimi nina mahaba na mchezaji fulani hilo lisikukwaze",amesisitiza mlezi wa timu hiyo.

"Nashukuru kwa wamiliki wa timu hii ambao ni Halmashauri ya Jiji la Mwanza kwa kuniamini kushika nafasi hii,nina wahaidi sitowaangusha katika kufikia malengo ya kucheza Ligi kuu msimu ujao,"Mbwana Makatta,Kocha Pamba Jiji FC

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza ambao ndiyo wamiliki wa timu hiyo,Aaron Karugumjuli amebainisha kazi iliyo mbele yao ni kumpa ushirikiano kocha huyo ili kukata kiu ya wana Mwanza ya kuona timu yao ikishiriki Ligi kuu.

"Kocha Mbwana ni mzoefu na amefundisha miaka ya nyuma timu ya hapa Mwanza ya Alliance,siyo mgeni na anarudi nyumbani kwa mara nyingine kuja kuinoa Pamba Jiji FC,karibu sana na tutakupa ushirikiano wa kutosha," Mhe.Sima Constantine Sima,Meya wa Jiji la Mwanza.

Timu ya Pamba Jiji FC mara ya mwisho kucheza Ligi kuu ni mwaka 1999 iliposhuka daraja.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.