• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA APINGA MKANDARASI MAJI BUTIMBA KUONGEZEWA MUDA BILA KULIPA FIDIA

Posted on: August 3rd, 2023


- Adai mamlaka na Wizara kumuongezea muda bila fidia  ni kinyume vha utaratibu na sheria

- Serikali mara zote imehaidi kwa wananchi mradi utakamilika Julai 31,2023

- Ataka mkandarasi akatwe fedha za fidia zaidi ya Bilioni 2 ili iwe fundisho.


Mkandarasi anayetekeleza  mradi mkubwa wa maji wa Butimba,Kampuni ya Sogea Satom kutoka Ufaransa ametakiwa kulipa adhabu ya kisheria ya malipo ya Shs bilioni 2.5 kutokana na kuzembea kukamilisha mradi huo kwa wakati na badala yake kuongeza muda kinyemela bila uongozi wa Mkoa kujulishwa.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.CPA Amos Makalla ametoa agizo hilo leo ikiwa ni ahadi yake aliyoitoa wakati wa ziara yake miezi michache iliyopita na kuahidiwa mradi huo kukamilika Julai 31,2023,amesema kitendo cha kuongezewa Mkandarasi miezi mitatu kinyemela ikiwa ni mara ya pili hakikubaliki na ni kwenda kinyume na maagizo ya Rais Samia Suluhu aliyetaka mradi huo kukamilika kwa wakati.

"Hiki kitendo narudia kusema hakikubaliki,ni lazima Mkandarasi huyu akatwe hiyo fidia ili naye fedha hizo zimuume kwani ni dhahiri hatambui wananchi wa Mwanza wanavyotaabika na kukosa huduma hiyo

 kwa muda mrefu",amesema CPA Makalla.

Ameiagiza Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jiji Mwanza,MWAUWASA kukaa na Wizara ya maji kuanza kutekeleza mara moja kumkata fedha hizo kwa muda huo wa miezi mitatu ili iwe fundisho kwa Wakandarasi  wengine wababaishaji.

"Hili jambo linashangaza sana Mkandarasi amelipwa fedha kwa asilimia 100 mimi nawahaidi wananchi kuanza kupata huduma ya maji ya uhakika kuanzia Julai 31 baada ya kuongezewa muda Februari mwaka huu,huyu Mkandarasi hana sababu yoyote ya kuongezewa muda lakini sasa ni lazima amalizie hiyo miezi 3 pamoja na adhabu hiyo malipo ya fedha kwa kweli sijaridhika kabisa ,"CPA Makalla.

"Mhe.Mkuu wa Mkoa sisi kama MWAUWASA tunakuahidi kuanzia Septemba 15 wananchi wa Mwanza wataanza kupata maji wakati Mkandarasi atakapoanza zoezi la majaribio,hivyo tunaamini changamoto ya ukosefu wa maji kwa wananchi itakwisha,"Mhandisi Robert Lupoja,Kaimu Mkurugenzi MWAUWASA.

Kampuni ya Sogea Satom imeanza kutekeleza mradi huo wa maji Butimba wenye gharama ya Shs bilioni 70 kuanzia mwaka 2021 huku uzalishaji wa maji kwa Mkoa wa Mwanza ukiwa ni lita milioni 90 kwa siku na mahitaji halisi ni lita milioni 160 kwa siku na kukiwa na upungufu wa zaidi ya lita milioni 60.






Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.