• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA ASHAURI TANROADS KUMUONDOA MKANDARASI WA BARABARA YA SENGEREMA- NYEHUNGE

Posted on: December 7th, 2023

RC MAKALLA ASHAURI TANROADS KUMUONDOA MKANDARASI WA BARABARA YA SENGEREMA- NYEHUNGE


*Amtaka TANROADS kumuondoa Mkandarasi anayejenga barabara hiyo na kumpata mwingine mara moja*


*Amempongeza Rais Samia kutoa fedha nyingi kwenye ujenzi wa Miundombinu mkoani humo*


*Amempongeza Mwenyekiti wa CCM kwa ushindi na amemuahidi ushirikiano wa Serikali*


*Awataka MaDC, MaDED,TANROADS na TARURA kudhibiti taka kwenye mitaro*


*Amewaelekeza Kamati za Usalama za Wilaya kwa kushirikiana na Kamati za Maafa kuwa tayari na majanga*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amewataka Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) kumuondoa mkandarasi AVM Dillingham aliyepewa kazi ya ujenzi wa barabara ya lami ya Sengerema - Nyehunge (54.4KM) kwa zaidi ya Bilioni 73 kutokana na kuchelewa kuanza ujenzi huo tangia Mwezi Agosti na apatikane mkandarasi mweingine anapatikana na kuanza kazi mara moja.

Mhe. Mkuu wa Mkoa ametoa agizo hilo mapema leo tarehe 07, 2023 wakati wa Kikao cha kwanza cha Bodi ya Barabara Mkoa kwa Mwaka wa 2023/24 kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa mahususi kwa ajili ya kujadili maendeleo ya sekta hiyo.


"Mhe. Rais ametuletea fedha nyingi sana kutekeleza miradi ya ujenzi wa miundombinu ya barabara ambayo nimeiona mwenyewe kwa macho nilipokua kwenye ziara ya kusikiliza kero, Mkandarasi wa ujenzi wa barabara ya Nyehunge- Sengerema kwa Bilioni 70 ameshapatikana lakini hajaanza kazi sasa naagiza TĂ€NROADS kumuondoa mara moja." Mkuu wa Mkoa.

Ameongeza pia miradi ya ujenzi wa barabara za Kayenze- Airport na Kwimba Magu ambazo zinaanza kujengwa kwa Kilomita 10 na Ngudu- Mabuki kwa Kilomita 3 pamoja na Bilioni 32 zilizotolewa kujenga vivuko vipya na kukarabati vya zamani sambamba na Bilioni 30 zilizotolewa za ujenzi wa Jengo la abiria katika kuufanya uwanja huo kuwa wa Kimataifa.


Vilevile, Mhe. Mkuu wa Mkoa Awataka TANROADS na TARURA kufanya usafi kwenye mitaro ili kuondoa takataka zinazozuia maji kutoririka vema kwenda ziwani ili kuweka hali ya usalama kwa kaya zisivamiwe na maji yanayotuama sehemu mbalimbali.

Kufuatia mvua kubwa zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali nchini, CPA Makalla amezitaka kamati za usalama za Wilaya kwa kushirikiana na kamati za maafa kuwa tayari kukabiliana na majanga yanayoweza kutokea hususani Elnino kwani tayari mikakati ilishawekwa kwa usimamizi wake.


Aidha, Mkuu wa Mkoa amempongeza Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Mwanza kwa ushindi wa kishindo alioupata kwenye Uchaguzi wa Chama hicho uliofanyika juma lililopita kufuatia kuhamishwa kwa mwenyekiti wa awali kwenda Masasi Mkoani Mtwara kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri.

Mhe. Michael Masanja, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza ametumia wasaa huo kuwashukuru wanachama wa chama hicho kwa kumchagua kwa kishindo kuwa Mwenyekiti kwenye uchaguzi na amewataka wadau wa sekta hiyo kuendelea kusimamia vema barabara na kulipa fidia kwa wakati kwenye miradi ya ujenzi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MAKUZI YA AWALI YA MTOTO MSINGI WA UJENZI WA TAIFA IMARA - RAS BALANDYA

    May 16, 2025
  • RC MTANDA AWAKARIBISHA MWANZA WANAFUNZI KUTOKA UGANDA

    May 15, 2025
  • RC MTANDA AKOSHWA NA BONANZA LA USHIRIKA NA MABENKI

    May 14, 2025
  • RAS MWANZA ATAKA UHAMASISHAJI CHAKULA CHENYE LISHE KUONGEZEKA SHULENI

    May 13, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.