• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA ATOA MAAGIZO KWA WAVAMIZI WA SHAMBA LA MIFUGO MABUKI-MISUNGWI

Posted on: January 18th, 2024

RC MAKALLA ATOA MAAGIZO KWA WAVAMIZI WA SHAMBA LA MIFUGO MABUKI-MISUNGWI


*Aagiza uongozi Mabuki, jeshi la polisi wilayani humo kufanya ukaguzi kubaini wavamizi wote*


*Asema Rais Samia anaziishi fikra za Mwl Nyerere kwa kutoa Ng'ombe jike (Mitamba) 500*


*Awapongeza wanafunzi  wa BBT kwa mafunzo mazuri ya ufugaji wa kisasa*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amelitaka jeshi la polisi wilayani Misungwi kwa kushirikiana na uongozi wa shamba la mifugo la Mabuki kuweka mipaka ya eneo lote la hekari elfu 25 na kuwabaini wavamizi ili mkuu wa wilaya hiyo awaondoe mara moja kwa ustawi wa shamba hilo.

Ametoa agizo hilo leo tarehe 18 Januari, 2024 wilayani Misungwi baada ya kupokea changamoto ya wananchi wakiwa na mifugo mingi kuvamia shamba hilo na kuathiri shughuli za utafiti, uzalishaji na Utoaji wa mafunzo kwa wafugaji jambo linalofanywa na wananchi kutoka kwenye kata nne zinazozunguka shamba hilo.

"Malengo ya kuanzishwa kwa taasisi hii na kuenzi fedha nyingi anazozileta Mhe. Rais Samia kwenye shamba hilo lazima ziwe na tija maana wavamizi ndio wanaotaka taasisi hii ife, vijana wa mradi wa BBT LIFE wasifanikiwe, mifugo yetu ife kwa magonjwa na hatutakubali kufika huko." CPA Makalla.


Aidha, amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutoa ng'ombe majike 500 (Mitamba) kwenye shamba hilo ambao wamesaidia kuendeleza uzalishaji na kutolea mafunzo kwa wafugaji ya namna bora ya kuzalisha nyama na maziwa bora kupitia mafunzo ya muda mfupi na mrefu yatolewayo shambani hapo.

Aidha, awapongeza wanafunzi walio kwenye shamba hilo chini ya mradi wa Jenga Kesho Bora (BBT) kwa mafunzo mazuri waliyoyapata na akabainisha kuwa uvumilivu wao utawasaidia kujiajiri kwa kufanya shughuli za uzalishaji kupitia ufugaji wa kisasa waliojifunza.


Mhe. Paul Chacha, mkuu wa wilaya ya Misungwi ametoa onyo kwa wafugaji wanaoingiza mifugo kwenye shamba hilo kuacha mara moja ili kuhakikisha utafiti, uzalishaji na mafunzo yanafanikiwa kwa mujibu wa sheria za uanzishwaji wa shmaba hilo la mifugo.

Meneja wa Shamba hilo Leni Mwala ametumia wasaa huo kumshukuru Rais Samia kwa kuendeleza shamba hilo lililoanzishwa mwaka 1967 lenye hekari elfu 25 kwa kuwaletea ng'ombe jike 500 (Mitamba) mwaka 2022/23 ambao wamesaidia kuendeleza wafugaji na kujifunzia.

"Serikali ya awamu ya Sita imetushangaza kwa furaha maana inatimiza maono ya Baba wa Taifa letu Hayati Rais Nyerere kwa kutuletea Mitamba 500 jike kwa ajili ya kuwakuza na kutumika kuendeleza kwenye utafiti kwa manufaa ya jamii ya wana Mwanza." Mwala.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MWANZA, SIMIYU ZANG'ARA UTAMILIFU DARASA LA SABA KANDA YA ZIWA

    May 30, 2025
  • RAS MWANZA AZINDUA RASMI MRADI WA KUPAMBANA NA UGONJWA WA SELI MUNDU

    May 30, 2025
  • WAANDISHI WA HABARI MWANZA WAPIGWA MSASA MIKAKATI YA KUTOKOMEZA WATOTO WA MITAANI

    May 29, 2025
  • RAS MWANZA AWATAKA VIONGOZI WA UMMA KUDUMISHA NIDHAMU NA UFANISI KAZINI

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.