• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA ATOA ONYO KWA WANANCHI WANACHUKUA SHERIA MKONONI NA KUHATARISHA USALAMA

Posted on: November 6th, 2023

RC MAKALLA ATOA ONYO KWA WANANCHI WANACHUKUA SHERIA MKONONI NA KUHATARISHA USALAMA


*Amewataka wananchi kufuata sheria na kutumia mahakama kuwasilisha madai yao*


*Awaagiza Kamati ya Usalama ya Wilaya hiyo kuweka mpango wa amani wakati wote*


*Atoa wito kwa wanaMisungwi kujiandaa na Fursa zitokanazo na Reli ya Kisasa*


*Amemshukuru Rais Samia kwa kujenga Mradi wa Maji utakaowanufaisha Misungwi*


Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amewataka wananchi kuacha kujichukulia sheria mkononi na kuhatarisha usalama kwa jamii  kutokana na tukio lililotokea mwezi Oktoba katika kijiji cha mwaniko Wilayani Misungwi la vijana wawili kuchomwa moto na kundi la wananchi wakidaiwa kuiba mpunga na kuku.

Mkuu wa mkoa Makalla  ametoa rai hiyo mapema leo Novemba 6, 2023 wakati akizungumza na wananchi kwenye mkutano wake wakati akisikiliza na kutatua kero za wananchi Wilayani Misungwi ikiwa ni ratiba yake aliyojipangia ya kuwafuata wananchi kwenye wilaya zote tangia alipozindua rasmi zoezi hilo mwezi Septemba mwaka huu.

Makalla amesema Mahakama ndicho chombo cha kisheria kinachotoa haki hivyo wananchi wanapokua na jambo wanapaswa kulifikisha mahakamani ili likasikilizwe na kupatiwa maamuizi ya kisheria na amefafanua kwamba zaidi ya wananchi 35 wamekamatwa kutokana na kujihusisha na tukio hilo ovu kwa watu wasio na hatia.

"Nitoe Onyo kwa wananchi kutochukua sheria mkononi, chombo kinachotoa haki ni mahakama hivyo nataka jambo hili lisijirudie tena na mabalozi, wenyeviti wa vijiji, watendaji wa vijiji na kata pamoja na viongozi wote tushirikiane kulinda amani" Makalla.

Aidha, amewaagiza Kamati ya Usalama ya Wilaya hiyo kuketi na viongozi wa ngazi zote kuanzia kwenye vitongoji kuwekeana mikakati ya kuhakikisha kunakua na amani wakati wote ndani ya vijiji, kata, tarafa na wilaya kwa ujumla.

Vilevile, Mhe. Makalla amewataka

wananchi wa Misungwi kuchangamkia fursa zinazoletwa na Mradi wa Reli ya Kisasa (SGR) kwani kwenye kituo cha Fella patakua ndipo kituo cha kupakia na kushusha mizigo kabla ya kusafirishwa kwenda kwenye mikoa na nchi za jirani.

Halikadhalika, Mhe. Makalaa ametumia wasaa huo kumshukuru Rais Samia kwa kujenga mradi mkubwa wa maji wa Butimba unaotarajia kuwapatia maji wananchi wa Misungwi na ujenzi wa barabara fupi ya kwenda Kahama unaotarajiwa kuanza siku za usoni.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.