• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA ATOA SIKU 42 KWA MKANDARASI KUKAMILISHA UJENZI WA AWAMU YA KWANZA YA JENGO LA HALMASHAURI KWIMBA.

Posted on: November 28th, 2023

RC MAKALLA ATOA SIKU 42 KWA MKANDARASI KUKAMILISHA UJENZI WA AWAMU YA KWANZA YA JENGO LA HALMASHAURI KWIMBA


*Asema Mkandarasi huyo hataongezewa tena muda wa ujenzi wa jengo hilo*


*Awaagiza Halmashauri hiyo kuondoa changamoto kwenye ujenzi huo kwa kufanya malipo kwa wakati*


*Amshukuru Rais Samia kwa kuidhinisha zaidi ya Bilioni 4 kujenga Makao Makuu hayo*


*Awapongeza Kwimba kwa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya, awaahidi Madaktari bingwa kutoa huduma hapo*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Makalla amemtaka Mkandarasi Kwiyera Interprises Limited kukamilisha ujenzi wa Jengo la Makao Makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba kufikia Disemba 31, 2023 ili awamu zingine za ujenzi ziendelee na kuwapatia watumishi na wananchi huduma nzuri.

Ametoa agizo hilo mapema leo akiwa kwenye ziara ya kukagua miradi ya maendeleo kwenye wilaya hiyo alipotembelea ujenzi huo unaofanyika kwenye kata ya Ngudu kwa zaidi ya Bilioni 4 ambapo bilioni 1.3 zitatumika kwa awamu ya kwanza.

"Mkandarasi leo umechelewa na umeshaongezewa mara nne muda wa kukamilisha nami kwa kuzingatia ucheleweshaji wa malipo ya fedha kwa mkandarasi huyo nakutaka sasa ukamilishe jengo ili hadi Disemba 30 mwaka huu." Mhe. Makalla

Aidha, Makalla amemshukuru Rais Samia kwa kutenga fedha zaidi ya Bilioni 4 kwa ajili ya ujenzi wa jengo hilo (Bilioni 1.3 awamu ya kwanza) ambalo amebainisha kuwa litasaidia kuwaweka watumishi kwenye mazingira nadhifu ya kufanyia kazi na wananchi kupata huduma safi.

Vilevile, amewaagiza idara ya ujenzi na Mkurugenzi wa halmashauri hiyo kusimamia ili mkandarasi awepo eneo la kazi wakati wote na kwamba asipo kamilisha hadi kufikia wakati huo atapewa adhabu kwa sheria na akamuahidi mkandarasi huyo kuwa ifikapo Januari 03, 2024 atafika kukagua.

Awali Mkuu wa Wilaya ya kwimba Mhe. Ng'wilabuzu Ludigija alifafanua kuwa Mkandarasi huyo amekua na mwenendo wa kusuasua kwenye ujenzi hadi kufikia hatua ya kuongezewa muda kwa mara tatu baada ya muda wa awali kuisha kwa mujibu wa mkataba pamoja na kupatiwa fedha.

Akikagua hali ya utoaji huduma kwenye  Hospitali ya Wilaya inayojengwa kwa zaidi ya Bilioni 3.8 kwenye eneo la Icheja kuanzia mwaka 2018/19 CPA Makalla amewapongeza Kwimba kwa kukamilisha ujenzi ambapo wagonjwa zaidi ya 475 wanalazwa kwa mwezi na kusaidia mtiririko wa huduma.

"Rais Samia Suluhu Hassan ametoa fedha za ujenzi na vifaa vya kisasa, tunatambua kazi nzuri inayofanywa na wataalamu wa afya ila lazima tusimamie matumizi ya lugha nzuri  kwa wagonjwa kwani inaleta matumaini hata kabla ya kuanza kutoa huduma yenyewe" Amesisitiza CPA Makalla.

Akitoa taarifa ya ujenzi huo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Happness Msanga amebainisha kuwa fedha hizo zilitoka kwa ajili ya ukarabati wa iliyokua hospitali ya wilaya eneo la kakora lakini kutokana na ufinyu wa eneo waliamua kujenga hospitali mpya kwenye kata ya Ngudu.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.