• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA AWAPANDISHA MZUKA PAMBA JIJI FC

Posted on: December 7th, 2023

RC MAKALLA  AWAPANDISHA MZUKA PAMBA JIJI FC


*Awamwagia noti wachezaji na benchi la ufundi kuelekea michezo miwili ya nyumbani*


*Awatia Shime mchezo dhidi ya TMA kutoka na ushindi nyumbani*


*Asema Pamba FC inastahili kukaa kwenye nafasi za juu katika msimamo wa Ligi ya Championship*


*Abainisha kuwaleta wachezaji  wanne kwa Majaribio kutoka Congo DRC kwenye Dirisha dogo la usajili*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla leo Disemba 7,2023 ameitembelea kambi ya timu ya soka ya Pamba Jiji FC inayoshiriki Ligi ya Championship na kuwapa motisha ya Shilingi Milioni 4, ambapo 3 kwa wachezaji na 1 kwa benchi la ufundi kutokana na kuwa na matokeo mazuri katika michezo yao ya hivi karibuni.

Akizungumza na wachezaji hao iliyopo kambini hapo kwenye Mtaa wa Iseni nje kidogo ya Jiji la Mwanza, Mkuu huyo wa Mkoa amewapongeza wachezaji hao kwa kupambana vizuri dimbani na kushika nafasi ya tatu ikiwa na mtaji wa pointi 27.

"Kwa hadhi ya Pamba Jiji nafasi tuliyonayo ya pili nikiwa na maana Jumapili hii tunashinda na kushika nafasi hiyo ndiyo tunastahili na tusishuke bali tupande juu, "amefafanua Mkuu huyo wa Mkoa ambaye ni mlezi wa timu hiyo.

Ameongeza kuwa wakati wa dirisha dogo atawaleta wachezaji wanne kutoka Congo DRC na kama dawati la ufundi litaridhika nao watasajiliwa kwa lengo la kuiongezea nguvu Pamba Jiji FC.

"Mhe Mkuu wa Mkoa tunaendelea kukuahidi kufanya vizuri katika michezo yetu na kutimiza lengo letu la kupanda Ligi kuu msimu ujao,tunakushukuru kwa kushikamana nasi,"Alhaji Majogolo,Mtendaji Mkuu wa Pamba Jiji FC.

Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza, ambaye ni Mkuu wa Kitengo cha TEHAMA ndugu Peter Leti amesema kambi ya timu hiyo inaendelea vizuri na maelekezo yote anayotoa wanayazingatia hali ambayo yameleta matokeo chanya hadi sasa.

Nahodha wa wana TP Lindanda Jerryson Tegete akipokea kitita cha Shs milioni 3 kwa niaba ya wachezaji wanzake kutoka kwa mkuu wa Mkoa,amesema watazidisha ari ya kufanya vizuri ili kutimiza nia yao ya kucheza Ligi kuu.

"Mhe Mkuu wa Mkoa mchezo wetu dhidi ya TMA nakuahidi tutafanya vizuri kwani kasoro ndogo za kiufundi upande wa umaliziaji nimeufanyia kazi," Mbwana Makatta kocha mkuu wa Pamba Jiji FC.

Timu ya Pamba Jiji FC itashuka dimbani Nyamagana Jumapili hii kumenyana na TMA inayotokea Arusha.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.