• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA AWATAKA USHIRIKA KUTOA ELIMU KWA WAKULIMA JUU YA FAIDA ZA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI

Posted on: January 11th, 2024

RC MAKALLA AWATAKA USHIRIKA KUTOA ELIMU KWA WAKULIMA JUU YA FAIDA ZA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI


*Awataka vyama vya ushirika kutoa elimu ya faida za mfumo huo*


*Amesema mfumo huo unatoa uhakika wa soko la mazao*


*Aziagiza Halmashauri kukutana na wadau wilayani*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amewataka Wadau wa ushirika kutoa elimu ya kutosha kwa wakulima juu ya faida za mauzo ya mazao kwa mfumo wa stakabadhi ghalani kwa maendeleo ya sekta hiyo.

Mkuu wa Mkoa ametoa maagizo hayo mapema leo Januari 11, 2024  wakati wa kikao cha wadau wa ushirika kilicholenga kujadili utekelezaji wa mfumo wa stakabadhi ghalani kwa mazao ya choroko na dengu 2023/24.

Amesema, wakulima wanataka kuona wanapata bei nzuri kwenye mazao kufuatia kuwekeza muda na nguvu kwenye kilimo kwa msimu mzima aidha kwa mikopo kutoka kwenye mabenki hivyo wanachohitaji ni kufahamishwa manufaa ya mfumo huo.

"Serikali inatambua mchango wa mfumo huu na umesaidia kuchochea wakulima kupata soko la uhakika lenye tija, mfumo huu umesaidia wakulima kwenye mazao kama kakao, korosho na ufuta na kwamba umekuza huduma za kifedha vijijini." Mkuu wa Mkoa.

Vilevile, amefafanua kuwa Mfumo wa stakabadhi ghalani una manufaa makubwa sana na umesaidia wakulima kutumia mzani halisi na kuongeza kipato kwa misimu miwili ya 2020 hadi 2022 na sasa Serikali imejipanga kuboresha zaidi huduma ili mkulima anufaike zaidi.

Robert Sunza kutoka Tume ya Maendeleo ya Ushirika nchini amesema wao kama wahamasishaji na wasimamizi wa maendeleo ya ushirika na kwenye mfumo huo unasaidia kupata ubora wa bidhaa, ushindani wa bei kutoka kwa wanunuzi na kupata takwimu za uhakika.

"Vilevile mfumo wa stakabadhi za ghala unasaidia kuongeza uzalishaji, mapato, miundombinu ya uhifadhi, usimamizi pamoja na kuimarika kwa biashara kutokana na kuongezeka kwa wanunuzi." Amefafanua ndugu Sunza.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTANDA ASISITIZA UIMARISHWAJI WA UMOJA NA MSHIKAMANO

    May 12, 2025
  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.