• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA AWATAKA WANANCHI WA NANSIO UKEREWE KUTUMIA MAJI SAFI NA SALAMA

Posted on: November 23rd, 2023

RC MAKALLA AWATAKA WANANCHI WA NANSIO UKEREWE KUTUMIA MAJI SAFI NA SALAMA


*Amshukuru Rais Samia kwa kutoa fedha zaidi ya Milioni 350 kuongeza Usambazaji Maji*


*Awataka MWAUWASA kutoa Elimu kwa wananchi kutunza mradi*


*Awashauri wananchi kuachana na mazoea ya kutumia Maji ya ziwani*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amewataka wananchi wa Nansio Ukerewe kutumia maji safi na salama kutoka chanzo na kituo cha tiba ya Maji Nebuye chenye thamani ya zaidi ya Bilioni 14. 8 ili kujihakikishia afya bora na kuepukana na Magonjwa ya tumbo yatokanayo na matumizi ya Maji ya ziwani.

Mhe. Makalla amesema hayo mapema leo novemba 23, 2023 wakati wa ziara yake wilayani Nansio alipotembelea Chanzo na Kituo cha Tiba ya Maji Nebuye kilicho kwenye Usambazaji wa zaidi ya Kilomita 23.2 kwa zaidi ya Milioni 350 chini ya Mamlaka ya MajiSafi na Usafi wa Mazingira Mwanza (MWAUWASA).


Makalla ametumia wasaa huo kumshukuru Rais Samia kwa kutoa fedha hizo ili kuboresha huduma hiyo kwa wananchi ambapo amebainisha kuwa hali ya upatikanaji wa Maji safi itaongezeka na wananchi wanapaswa kuchangamkia fursa hiyo kwa kuunganisha maji kwenye nyumba zao na kuachana na matumizi ya Maji ya ziwa.

"Maji haya ndio safi na Salama kwani yametibiwa hivyo hakuna tena magonjwa ya tumbo tukiyatumia kwa hiyo nawasihi tuachane na maji ya ziwa ambayo si salama kwa matumizi na hatarishi kwa wananchi kuliwa na mamba na viboko" Makalla.


Halikadhalika, Makalla amewataka MWAUWASA kutoa elimu kwa wananchi wa Nansio ili waumiliki mradi wao na kuweza kuutunza wakijivunia kuwa Rais Samia anauboresha kwa ajili yao hivyo wanapaswa kuutunza ili uwe na tija.

Mkurugenzi wa Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira (MWAUWASA) Mhandisi, Robert Lupoja amebainisha kuwa chanzo hicho cha maji kinahudumia wateja 3900 kwa sasa kwenye vituo vya maji 52 na kwamba wapo kwenye juhudi za kuondoa kabisa upotevu wa maji wa asilimia 10 uliopo kwa sasa.

"Wananchi wa Nansio tunaenda kuwaongezea huduma ya maji safi kupitia usambazaji huu mkubwa utakaotufikisha kwenye kuhudumia wananchi hadi kufikia asilimia 95 ifikapo mwaka 2024/25 hivyo tunawaomba mlipe ankara za maji kwa wakati ili tuongeze usambazaji." Amesisitiza Mkurugenzi huyo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.