• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA AZINDUA MIUNDOMBINU YA KIDATO CHA TANO MWAMASHIMBA SEKONDARI, KUSAIDIA KUONDOA MSONGAMANO DARASANI NA BWENINI

Posted on: November 28th, 2023

RC MAKALLA AZINDUA MIUNDOMBINU YA KIDATO CHA TANO MWAMASHIMBA SEKONDARI, KUSAIDIA KUONDOA MSONGAMANO DARASANI NA BWENINI


*Aupongeza uongozi wa shule hiyo na Halmashauri kwa usimamizi mzuri wa ujenzi*


*Awataka wanafunzi kutumia uboreshaji wa miundombinu kusoma kwa bidii kuongeza ufaulu*


*Aagiza kulinda eneo la shule hiyo kwa kutambua mipaka na kuweka uzio*


*Awataka wazazi kupeleka watoto shule wakapate elimu na sio kuwaacha nyumbani*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla leo Novemba 28, 2023 amezindua miundombonu ya kidato cha tano kwenye Shule ya Sekondari Mwamashimba wilayani Kwimba iliyogharimu zaidi ya shilingi Milioni 600.

Akizungumza na wanafunzi wa shule hiyo, Mhe. Makalla amewapongeza uongozi wa shule hiyo na halmashauri kwa usimizi mzuri wa Mabweni 3, vyumba vya madarasa 8 na Matundu ya vyoo 13 utakaosaidia kupunguza msongamano wa wanafunzi kwenye madarasa na mabweni.

"Nimeona mabweni mazuri yenye mpangilio mzuri wa vitanda, madarasa na matundu ya vyoo vyote kwenye hali ya usafi na unadhifu mzuri, tumieni jitihada hizi za uboreshaji kutulia na kusoma kwa bidii na nina imani baadae tutawapata viongozi wazuri kutoka kwenye shule hii." Makalla.

Vilevile, Mhe. Makalla ameagiza kulindwa kwa eneo la shule hiyo kwa kutambua na kuweka mipaka na kuweka uzio ili kuwalinda wanafunzi na kuepusha migogoro ya ardhi inayosababishwa na wananchi kuingia kwenye maeneo ya taasisi hususani yasiyo na mipaka inayofahamika.

Mhe. Ng'wilabuzu Ludigija amemhakikishia kiongozi huyo wa Mkoa kuwa ufaulu utqongezeka kwani pamoja na kuondoa msongamano wanafunzi kwenye shule hiyo watapata fursa nzuri ya kusoma kwenye mazingira mazuri ya kufundishia na kujifunzia.

"Mhe. Mkuu wa Mkoa wanafunzi wa kidato cha tano na sita wapo zaidi ya Mia 600 lakini kwa uwepo wa mabweni haya hivi sasa kila mwanafunzi atalala kwenye kitanda chake, hakuna tena msongamano bweni wala darasani." Amefafanua Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Bi. Happness Msanga.

Katika hatua nyingine, Mkuu wa Mkoa amezindua Shule mpya ya Msingi Mwalulyeho katika kijiji cha Chasalawi, Bupamwa- Mwamashimba iliyojengwa kwa zaidi ya Milioni 250 ambayo imesaidia kuondoa adha ya kutembea umbali wa zaidi ya Kilomita 4.5 kuelekea shule ya Chasalawi.

"Kama mlikua na kiu ya kupata shule, sasa mmejengewa tumeiona ni nzuri yenye samani za kutosha, basi waleteni watoto kwenye hii shule wasome maana hawa 303 wamehamia hivyo wazazi hakikisheni watoto wote wanakuja shule ifikapo mwezi Januari 2024 asibaki nyumbani hata mmoja mweye umri wa kuanza shule. Mkuu wa Mkoa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.