• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Makalla azindua msimu mpya wa Pamba, awataka Maafisa Ugani kuwa na shamba darasa

Posted on: November 17th, 2023

*RC Makalla azindua msimu mpya wa Pamba, awataka Maafisa Ugani kuwa na shamba darasa*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla leo Novemba 17,2023 amezindua msimu mpya wa Pamba 2023-24 wilayani Magu na kuwataka Maafisa Ugani wote Mkoani humo kuwa na shamba darasa kwa lengo la kuongeza tija wakati wa mavuno.

Akizungumza kwa niaba yake Katibu Tawala Msaidizi Uchumi na Uzalishaji Emil Kasagara kwenye  kijiji cha Mwalina kata ya Mwamabanza ulikofanyika uzinduzi huo, amesema Serikali imeweka mazingira rafiki kuanzia kwa Maafisa Ugani kwa kuwapatia nyenzo ya usafiri wa Pikipiki hivyo ni wajibu wao kuhakikisha malengo ya kupata mavuno zaidi yanafikiwa.

"Malengo ya Mkoa wetu msimu huu huu wa 2023-24 ni kulima hekta 60,178 kupata mavuno ya tani 45,457,mpango huu utakuja na matokeo chanya endapo wakulima watapata elimu ya kutosha kutoka kwenu wataalamu",Kasagara.

Amewataka wakulima wa Pamba kuzingatia ushauri wa kitaalamu huku Serikali ikiwa tayari imewawekea mazingira mazuri kuanzia bei nafuu ya mbolea na mbegu bora na kuwasisitiza  kuondokana na ukulima wa kimazoea ambao matokeo yake ni kuvuna Pamba hafifu na zisizo na ubora.

Kwa upande wake kaimu Mkurugenzi wa bodi ya Pamba James Shimbe amebainisha msimu huu wamehakikisha kila kitu kimefika kwa wakati kwa mkulima ili afanye maandalizi mazuri ya Kilimo cha Pamba.

"Hadi kufika tarehe 15,Novemba 2023 jumla ya tani za mbegu ya Pamba 1,682 zimepelekwa kwenye Halmashauri zinazolima Pamba kati ya hizo Tani 1,394 zimegawiwa kwa wakulima",Shimbe

"Tumekuwa na mafanikio katika kilimo cha Pamba kwa misimu 3 mfululizo ikiwemo Pembejeo kuletwa kwa wakati,uzalishaji kuongezeka mwaka hadi mwaka kuanzia 2019 hadi 2023, na kuimarika kwa huduma za Ugani,"Emmanuel Siyo,mratibu wa zao la Pamba Mkoa wa Mwanza.

Mkoani Mwanza zao la Pamba linalimwa zaidi kwenye Halmashauri za Misungwi,Magu,Kwimba,Sengerema na Buchosa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.