• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA ZIARANI SENGEREMA APONGEZA UJENZI WA MIRADI, AHIMIZA WAZAZI KUPELEKA WATOTO SHULE

Posted on: January 15th, 2024

RC MAKALLA ZIARANI SENGEREMA APONGEZA UJENZI WA MIRADI, AHIMIZA WAZAZI KUPELEKA WATOTO SHULE


*Awapongeza Halmashauri kusimamia ujenzi wa madarasa kwa muda mfupi*


*Awataka wananchi kuchukua tahadhari ya Kipindupindu, aagiza kutolewa elimu*


*Awataka viongozi kushirikiana kuhamasisha wazazi kupeleka watoto shule*


*Awataka wananchi kulipa kodi kwa mujibu wa sheria kwa ajili ya maendeleo*


*Awapongeza TANROADS kuunganisha wananchi kupitia daraja la Bugakala*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema kwa kutekeleza ujenzi wa miundombinu ya madarasa kwa ubora na ufanisi mkubwa hususani shule mpya za Sekondari kwenye kata za Misheni na Nyampulukano.


Mhe. Makalla ametoa pongezi hizo leo Januari 15, 2024 wakati alipokua wilayani humo kwa ukaguzi wa miradi ya maendeleo, uandikishaji wa wanafunzi na ufuatiliaji wa maagizo yake aliyoyatoa wakati wa ziara yake ya kusikiliza kero za wananchi, kufuatilia uandishikishaji wa wanafunzi na kukagua miradi ya maendeleo.

Makalla amesema pamoja na ujenzi huo amebaini kuwepo kwa shule zilizosajili wanafunzi wengi hadi kwa asilimia 106 lakini uwepo wa shule zenye idadi ndogo ya wanafunzi waliosajiliwa kujiunga kidato cha kwanza, darasa la kwanza na awali na kufuatia hali hiyo ameagiza walimu kufanya uhakiki na kushirikiana na wazazi kuhakikisha watoto wanawasili shule.

Akiendelea na ziara hiyo kwenye miradi mbali mbali Mhe. Mkuu wa mkoa amewataka TARURA na TANESCO kufanya tathmini ya gharama za kupeleka huduma hizo kwenye shule mpya na kuwasilisha kwenye uongozi wa halmashauri ya Sengerema ili iweze kulipia na kuhakikisha maabara, madarasa na miundombinu mingine inapata huduma safi.

Vilevile, ametumia wasaa huo kuwataka viongozi na watendaji wilayani humo kushirikiana katika kutoa elimu kwa jamii ya maradhi ya ugonjwa wa kipindupindu na kuhakikisha kila anapopatikana mgonjwa mwenye dalili hizo basi apelekwe hospitali mapema iwezekanavyo akapate huduma hiyo ya bure huku akibainisha kuwa kuna wagonjwa 74 na mmoja akifariki.

Akikagua ujenzi wa jengo la Mamlaka ya mapato linalojengwa kwa zaidi ya Bilioni 2.3 wilayani humo, Mhe. Mkuu wa Mkoa amewataka taasisi hiyo kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kulipa kodi kwa hiyari na kuwataka wao kama watendaji kutenda haki katika kukisia na kutoza kodi huku akibainisha kuwa mkoa huo unaoshika nafasi ya pili Kitaifa kuchangia pato la Taifa umekusudia kukusanya zaidi.

Halikadhalika, amewapongeza TANROADS  kwa kuwaunganisha wananchi wa Sengerema na Nyangh'hwale mkoani Geita kupitia daraja la Bugakala lililojengwa kwa Milioni 650 ambapo amesema lilisababisha hadi vifo kutokana na kina kirefu cha maji na kwamba daraja hilo jipya litasaidia kusafirisha mazao na biashara.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.