• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malima afungua mafunzo ya ununuzi wa Pamba kidijitali

Posted on: February 22nd, 2023


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Adam Malima amewataka viongozi na wataalamu wanaotoa  elimu ya mfumo wa manunuzi ya Pamba kidijitali  kuhakikisha elimu hiyo inawafikia wadau wote ili kuondokana na malalamiko mbalimbali ya wakulima kuhusu kupunjwa uzito,wizi na kucheleweshewa fedha za malipo.

Mhe.Malima ameyasema hayo mara baada ya kufungua kikao hicho na kusema kuwa mfumo wa kidijitali kwenye shughuli za kilimo unaenda kuongeza usimamizi, ufanisi na upatikanaji wa takwimu sahihi kwa ajili ya mpango wa bajeti na uendelezaji wa sekta ya kilimo.

"Wakati tunaenda kuhamasisha matumizi ya mfumo huu wa kidijitali ni muhimu kuendelea kutoa elimu kwa wakulima, viongozi wa vyama vya ushirika, Serikali za mitaa na wataalamu wa kilimo na wadau wa pamba ili kujenga uelewa wa pamoja na uwezo wa matumizi ya vifaa mbalimbali vya kidijitali," amesema Mhe.Malima.

Mifumo hii inakwenda sambamba na kurahisisha malipo ya fedha kwa wakati kwa wadau mbalimbali hivyo ni hamasa kwa wakulima kufungua akaunti ili kurahisisha malipo kufanyika kwa wakati, amesisitiza.

Naye Mkaguzi wa Pamba wa Kanda ya Magharibi (TCB) Bw.Ally Mabrouke amesema kuwa kinachofanyika ni kurahisisha utaratibu uliokuwa ukitumika awali,ambapo kwa sasa zilizile taratibu zimerahisishwa na kuwekwa katika mfumo mmoja,na kusikiliza kuwa badala ya kutumia makaratasi kila kitu kitakuwa kwenye mfumo rasmi uliorahisishwa.

Kwa upande wake mwenyekiti wa chama cha Ushirika Shinyanga (SHIRECU) Kwiyolecha Nkilijiwa amesema anatamani Mkulima wa pamba ajivunie kilimo hiki kwani kwa sasa hawawezi hata kujenga nyumba nzuri ,na kusisitiza kuwa mfano huo utakapoanza kutumika inaonekana utamsaidia mkulima kwa kupata manufaa katika kazi yake.

Mhe. Malima ameongeza kuwa kwa msimu wa mwaka 2022/2023 uzalishaji wa pamba ulikuwa ni kilogramu 15,948,790 zenye thamani ya 26,688,226,722 kwa msimu ujao wa mwaka 2023/2024 Mkoa umelenga kuzalisha na kuuza kilogramu za pamba ghafi zipatazo kilo 56,007.12 na kupelekea matarajio ya zao la pamba kuongezeka kila mwaka kutokana na mpango wa Serikali katika kuinua Sekta ya Kilimo hususani mpango huu mpya wa mauzo ya Pamba kidijitali.

Kikao cha kujadili mfumo mpya wa mauzo ya Pamba kwa njia ya kidijitali kimefanyika katika ukumbi wa Kipepeo Mwanza Hoteli na kujumuisha wanunuzi wa zao la pamba, Bodi ya Pamba Tanzania, Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania, Bodi ya Usimamizi wa stakabadhi za ghala na soko la bidhaa Tanzania.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.