• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malima ahimiza kukamilika kwa wakati na ujenzi bora wa madarasa na Ofisi za walimu Mkoani Mwanza

Posted on: December 18th, 2022


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Adam Malima leo amefanya ziara ya ukaguzi wa ujenzi wa madarasa akianzia Wilaya za Nyamagana,Ilemela na Magu na kuhimiza ujenzi bora na kumalizika kwa wakati kabla ya mwaka huu kumalizika.

Mkuu huyo wa Mkoa akianzia ziara hiyo Wilayani Nyamagana shule ya Sekondari Mirongo amekagua ujenzi wa madarasa ya maghorofa na kutaka ofisi za walimu zisiwe mbali na madarasa hayo ili kudumisha nidhamu kwa wanafunzi na uwepo mzuri wa uwiano wa matundu ya vyoo na idadi ya wanafunzi.

"Noana maendeleo mazuri ya ujenzi wa madarasa lakini hili la ofisi za walimu kuwa mbali sijafurahishwa nalo kabisa,kila baada ya madarasa matatu lazime iwepo ofisi ya walimu ndiyo ujenzi wa kisasa ninao utaka" Mhe.Malima

"Wilaya ya Nyamagana tumepokea Shs Bilioni 3.92 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa 196,ambapo 130 yatakuwa ya chini na 60 ya ghorofa na madarasa yote yapo hatua za mwisho kukamilika kabla ya Disemba hii,tunatarajia kuwapokea Januari mwakani wanafunzi wote waliofaulu mwaka huu" Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mhe Amina Makilagi.

Aidha Mhe Malima akiwa Wilayani Nyamagana amekagua mradi wa barabara ya Unguja A ya mita 372 iliyogharimu Shs milioni 295 chini ya Mkandarasi Nyanza Road Works ambayo utekelezaji wake umefikia asilimia 73 ukigharimiwa na mfuko wa barabara

"Sisi Wilaya ya Ilemela tumepokea Shs Bilioni 2.2 za ujenzi wa madarasa 110,tayari 88 yamekamilika na 22 yapo hatua ya ukamilishaji,mahitaji yalikuwa madarasa 252 lakini tumejenga jumla 2548"Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ilemela Injinia Modest Apolinary.

Huko Wilayani Magu Mhe.Malima amefanya ukaguzi wa barabara ya Kisesa-Bujora yenye urefu wa Kilomota 1.72 inayojengwa na Mkandarasi Mangi Construction Ltd Kwa gharama ya zaidi ya Shs Bilioni 1 iliyo chini ya TARURA lakini inakabiliwa na changamoto ya uwepo wa mawe makubwa ardhini na kusua sua kwa kuondolewa nguzo za Tanesco na minara ya Kampuni za simu.

"Mmeniambia hii barabara mnatarajia kunikabidhi Mei 6 mwakani,sasa hizi changamoto nataka kesho mzizungumze kwa kina kikao cha bodi ya barabara ili nami nijue eneo langu kama Mkuu wa Mkoa nazitatuaje" amesisitiza Mkuu wa Mkoa

"Tumepokea zaidi ya Shs Bilioni 1 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa 163 ujenzi upo hatua ya asimia 82 na madarasa 26 yapo hatua ya ukamilishaji na mengine yamekamilika tunatarajia Disemba 22 mwaka huu madarasa yote kuwa tayari"Mkurugenzi wa Halmashauri ya Magu Fidelica Myoveka.

Mkoa wa Mwanza umepokea zaidi ya Shs Bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa Wilaya zote zilizopo ndani ya Mkoa huo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.