• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malima aiambia kamati ya Bunge Maji,Mifugo na Uvuvi umuhimu wa mradi wa Maji Butimba kwa Mkoa wa Mwanza.

Posted on: January 13th, 2023


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima leo Januari 13, 2023 ameipokea Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji ikiwa ziarani kukagua Mradi mkubwa wa Maji Butimba unaosimamiwa na Mamkala ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mwanza (MWAUWASA) wenye thamani ya Bilioni 69.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Almas Maige akimuwakilisha Mwenyekiti wa kamati hiyo amesema wamefika Mwanza kukagua Mradi wa Maji wa Butimba kujionea ni kwanini mradi huo haujaanza kutoa huduma ya maji  Disemba mwaka jana kama Makamu wa Rais alivyoagiza.

"Kamati hii inafanya kazi kubwa na kwa mafanikio makubwa sana na Wizara yetu imetumia sana Ushauri wa kamati hii kila wakati katika kuendeleza Sekta ya maji nchini, nakuahidi Mhe. Mkuu wa Mkoa vifaa vitafika ndani ya muda kutoka Ufaransa ili mradi ukamilike na nakuahidi kuwa tatizo la kutolewa maji kwa zamu mwanza litakwisha" Naibu Waziri wa wizara ya Maji Mhe. Maryprisca Mahundi.

Mhe. Malima ametumia wasaa huo kuwakaribisha wajumbe wa kamati hiyo na amebainisha kuwa Mradi wa Maji wa Maji Butimba ni mradi wa kimkakti kwa kuwa unakuja kutatua Changamoto kubwa ya maji na upo kama kielelezo cha Maendeleo ya kiuchumi kwa wananchi na Sekta hiyo mkoani humo.

"Mahitaji ya Maji kwa watu wa Mwanza ni Lita milioni 160 na mradi wetu mkubwa unaofanya kazi kwa sasa unazalisha Lita milioni 90 na sasa ukitoa maji yanayopotea wakati wa Usambazaji ambayo ni wastani wa lita milioni 32 tunapata maji lita milioni 65 kwa siku, hivyo mradi wa Butimba ambao unatarajia kuzalisha lita Milioni 48 utakua msaada mkubwa." Amefafanua Malima.

Vilevile, amejinasibu kuwa mkoa huo unatekeleza miradi ya Maji yenye thamani ya takribani Bilioni 300 na akatoa wito kwa MWAUWASA kudhibiti upotevu wa Maji ili uzalishaji uendane na usambazaji hivyo wañanchi waondokane na kero ya upungufu wa huduma hiyo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.