• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malima aiomba Wizara ya Afya kujenga Hospitali nyingine ya Rufaa Mwanza

Posted on: January 5th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Adam Malima ameiomba Serikali kupitia Wizara ya Afya kuona namna ya kujenga Hospitali ya Rufaa ingine mkoani humo ili kuondoa msongamano kwenye hospitali za Bugando na Sekou Toure kutokana na ongezeko kubwa la watu kanda ya ziwa.

Amebainisha hayo leo alhamisi (Januari 05, 2023) wakati akifunga kikao cha wadau wa Afya kilichofanyika kwenye ukumbi wa Mkuu wa Mkoa kilichoongozwa na Prof. Abel Makubi Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya wakati akihitimisha ziara ya Utoaji Elimu kuhusiana na muswada wa bima ya Afya kwa wote unaokwenda kujadiliwa bungeni siku za usoni.

Ameongeza kuwa katika kuboresha huduma za magonjwa ya Saratani Uongozi wa Mkoa umepeleka mapendekezo kwa Wizara ya afya kukipandisha hadhi kitengo cha kuhudumia magonjwa ya Saratani kwenye Hospitali ya Kanda Bugando kuwa hospitali kamili kutokana na waathirika wengi wa tatizo hilo wanatoka kanda ya ziwa.

Vilevile, amesema Mkoa umeiomba wizara kuleta Madaktari Bingwa kwenye Hospitali inayojengwa Wilayani Ukerewe kwa hadhi ya Rufaa ya Mkoa kuhakikisha vifaa tiba na wataalamu wapatikana ili wananchi waishio visiwani wapate huduma za kibingwa wilayani Ukerewe.

Katibu Mkuu Wizara ya Afya Prof. Abel Makubi amesema Serikali iko mbioni kuboresha huduma za afya kwenye kitengo cha Saratani katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando na ukamilishaji wa haraka utafanyika kwenye Hospitali yenye hadhi ya Rufaa ya Mkoa inayojengwa Nansio-Ukerewe.

"Nia ya Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha wananchi wanapata huduma za afya jirani na kwenye makazi yao, hivyo tunakwenda kuboresha huduma za Saratani Bugando maana kwa sasa pale kuna mashine moja ambayo haitoshi" Amesisitiza Prof. Makubi.

Aidha, amesema Wizara ya Afya inaendelea kutoa Elimu ya Bima ya Afya kwa wote kwa wananchi kuanzia ngazi za kitongoji hadi Taifa ili kuhakikisha wananchi wote wanapata uelewa wa suala hilo ambalo siku za karibuni litafikishwa bungeni kwa ajili ya kupata muswada ambao baadae utakua sheria rasmi.

Prof. Makubi ametoa rai kwa viongozi nchini kushirikiana na wizara hiyo katika kutoa Elimu na amewataka kuwa mbegu bora itakayofikisha Elimu ngazi za chini kupitia wadau na wataalamu wa afya nchini kwa kushirikiana na wana habari na kwamba mpango huu utakua na gharama za chini zaidi ya hali ilivyo kwenye bima za sasa.

Mjumbe wa Sekretarieti ya Bima ya Afya kwa Wote nchini, Bi. Jackine Tarimo amesema Chimbuko la kuanzishwa kwa muswada huo ni kutimiza wajibu wa Serikali kikatiba wa kuhakikisha wananchi wote wanapata huduma bora za afya bila kikwazo.

"Uhalisia unaonesha kuwa na idadi kubwa ya wananchi (asilimia 85) hawana bima za afya na hivyo kukosa uhakika wa kupata huduma za afya pindi zinapohitajika lakini kwa muswada huu utaonesha kuwa wananchi wote hasa wasio na uwezo watapata fursa ya kuingia kwenye huduma za Bima." Amesema Tarimo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. July 29, 2022
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2022 July 03, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI ICAP October 21, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC Malima awataka Madiwani kusimamia na kuendeleza vyema rasilimali za Bonde la Ziwa Victoria

    March 31, 2023
  • RC Malima awahimiza Wana Mwanza kufurika Dimbani Nyamagana Jumamosi hii kuwashangilia wana TP LINDANDA Pamba FC dhidi ya Kitayose

    March 30, 2023
  • Makinda awataka wasomi na wananchi kuyatumia matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi kujiinua kiuchumi

    March 29, 2023
  • RC Malima ahimiza kutokomeza unyanyasaji wa kijinsia

    March 27, 2023
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 33180, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras.mwanza@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.