• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malima akabidhi Viti. mwendo 70,Fimbo 30 kwa wenye mahitaji maalum Mwanza

Posted on: February 27th, 2023


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima amekabidhi Baiskeli 70 na Fimbo 30 kwa watu wenye mahitaji maalum vilivyotolewa na Mhe. Furaha Matondo Mbunge wa Viti Maalum Mkoani Mwanza kutoka Jimbo la Ukerewe Mkoani humo.

Akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi Vifaa hivyo iliyofanyika mapema leo Jijini Mwanza, Mhe. Malima amekemea tabia ya Unyanyapaa inayofanywa na baadhi ya watu kwa watu wenye Ulemavu na badala yake amewataka kuwapa nafasi ya kushiriki kujenga nchi katika vitu tofauti ambavyo wana vipaji navyo.

Vilevile, amemshukuru Mhe. Matondo kwa msaada huo na amemtia moyo kuendelea kuwajali wenye Ulemavu na akatoa wito kwa wengine kujitoa kwa kundi hilo muhimu na kwamba kwa Mwenyezi Mungu amefanya hisani yenye Ibada ndani yake.

Aidha, amewakemea wazazi na viongozi wanaonyamazia matukio ya ukatili wa kijinsia yanayotokea kwenye jamii na akawataka kuona kama ni jukumu la kila mmoja kukemea matendo kama ya ulawiti, ukatili na Unyanyasaji wa jamii ili kutokomeza madhira hayo kwenye jamii.

"Watoto wananyanyaswa sana, ulawiti na ubakaji vimekithiri sana nami nimehuzunishwa sana na matukio ya ukatili wa kijinsia na kwa watoto wadogo alafu jamii inawajua waovu hawa kwakuwa wanaishi nao" Ameongea Mhe. Malima wakati akionya kuhusiana na Ukatili wa kijinsia.

Mhe. Jamal Babu Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa akiwakilisha Mkoa wa Mwanza ametoa wito kwa Serikali kuendelea kuwajali watu wenye ulemavu nchini kwa kuwapa kipaumbele kwenye huduma na kuwawekea Miundombinu rafiki kwa matumizi hususani kwenye Shule na Zahanati.

Naye Mhe. Furaha Matondo amesema anamshukuru Mwenyezi Mungu kwa kumjalia kupata vifaa hivyo na kusaidia watu wenye uhitaji na hiyo yote amefanya kwa moyo wa dhati ikiwa ni kumsaidia Mhe. Rais katika kuboresha maisha kwa makundi ya watu wenye Ulemavu.

Bi. Neofita Mkiringi, Mtaalamu wa Viti Mwendo kutoka CCBRT ametoa wito kwa viongozi wanaotaka kutoa misaada ya Viti Mwendo kuwashirikisha wataalam wa Magonjwa ya viungo kabla ya kufanya hivyo ili kuwalinda watumiaji na matatizo ya vidonda Mkandamizo, Mgongo kupinda na miguu kuumia.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.