• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malima apokea mtambo wa kuchimba Visima,aishukuru Serikali ya Rais Samia

Posted on: March 3rd, 2023


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima amekabidhiwa mtambo wa kisasa wa kuchimba Visima na Malambo yenye thamani ya Shs milioni 550 ambayo itaanza kuchimba Visima 83 kwenye baadhi ya maeneo Mkoani humo.

Akizungumza katika hafla fupi ya kuwakabidhi mitambo hiyo kwa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) iliyofanyika Wilayani Misungwi, Mhe.Malima amesema licha ya Mkoa wa Mwanza kuwa na rasilimali kubwa ya maji ya Ziwa Victoria lakini kuna baadhi ya maeneo wananchi hawapati huduma hiyo hivyo mtambo huo ni ukombozi wa kumtua ndoo kichwani mwanamke.

"Kwa niaba ya wananchi wa Mwanza natoa shukran kwa Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan ambaye ameonesha upendo wa dhati wa kuendelea kuwapigania maendeleo wananchi wake,nawaomba sana tuitunze na tuitumie kwa malengo yaliyokusudiwa mitambo hii".Amesisitiza Mkuu huyo wa Mkoa.

"Mhe.Mkuu wa Mkoa bado tunaendelea kupambana kuhakikisha huduma ya maji vijijini  tunafikia asilimia 85 na mijini 95 hadi kufika mwaka 2025 kwa mujibu wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi inavyotutaka".Mhandisi Godfrey Sanga.Meneja RUWASA Mkoa

Amesema uchimbaji wa Visima 83 kwa bei ya Mkandarasi ingefikia Shs.2,554,265,406 lakini kwa kutumia mitambo hii  wanatarajia kutumia Shs.2,118,575,000 hivyo wameokoa Shs.435,690,406.

Mitambo hiyo ya kuchimba Visima imesambazwa Mikoa yote 25 ya Tanzania Bara iliyogharimu zaidi ya Shs Bilioni 15.

Aidha Mkuu huyo wa Mkoa akiwa njiani kwenda kukagua miradi ya maji huko Ihelele Wilayani Misungwi amepita kwenye shamba la Uzalishaji Mifugo la Mabuki na kutoa maelekezo kwa Maafisa Mifugo wote kutoka Halmashauri kukutana kwa ajili ya kuweka mkakati wa kujifunza namna ya ufugaji wenye tija wa kuwa na Mifugo michache yenye ubora na kumuingizia kipato mkulima.

"Nimepita hapa nami kuna somo nimelipata ambalo ni lazima wasaidizi wangu waje hapa kujifunza ili wakamsaidie mfugaji namna ya kujiongezea kipato kwa ufugaji wa kisasa".Amesema Mhe.Malima.

"Shule hii ya Sekondari ya wasichana ya Mwanangwa inayojengwa na TASAF, naendelea kusisitiza Miradi hii yote iwe imekamilika mwishoni mwa Machi mwaka huu kama tulivyoahidi kwa Waziri Mhagama kuwa tutamaliza Miradi yote ya TASAF kabla ya Aprili hasa baada ya kuonesha kuwa nyuma kukamilisha Miradi mingi licha ya fedha kutolewa zote na kuwa hatarini Mkoa wetu kukosa fedha nyingine awamu ijayo ya TASAF" Amehimiza Mhe. Malima alipopita kukagua shule hiyo itakayoanza Januari mwakani.

TASAF imetoa jumla ya Shs milioni 683,005,234.74 kukamilisha mradi wa shule hiyo.

Akiwa kata ya Nyamahiza kusikiliza kero za Wananchi, Mkuu huyo wa Mkoa ameiagiza  RUWASA na TANESCO kuwaharakishia Maendeleo wananchi kwa kuwaletea huduma haraka na kuwataka walimu wa shule ya Sekondari Magufuli kufuata taratibu za Utumishi wa umma baada ya kupata taarifa za kuwepo upungufu wa walimu ambao wameondoka huku wakitoa visingizio visivyo na tija.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.