• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malima asaini Mkataba wa Lishe baina yake na Wakuu wa Wilaya za Mwanza

Posted on: October 28th, 2022

*RC Malima asaini Mkataba wa lishe baina yake na Wahe.Wakuu wa Wilaya*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Adam Malima leo Octoba 28 ameongoza zoezi la utiaji saini wa Mikataba ya Afua za Lishe  baina yake na Wahe. Wakuu wa Wilaya saba zilizopo mkoani humo.

Akizungumza kabla ya kutia saini mikataba hiyo, Mhe.Malima amewataka Wahe.Wakuu wa Wilaya hizo  kuhakikisha wanaisoma na kuielewa ili waweze kuifanyia kazi kikamilifu kama ambavyo imekusudiwa na Serikali.

" Nawaombeni Wahe. Wakuu wa Wilaya  isomeni na kuielewa siyo kuisoma tu kwa kuwa mkiielewa mtaifanyia kazi na matokeo tutayaona ila mkiisoma tu mtaiacha hapo hapo," amesema Mhe.Malima.

" Chakula cha Lishe hakitakiwi kuwa na gharama kubwa... sasa nawaambia Wahe.Wakuu wa Wilaya nendeni mkatoe Elimu ya Lishe ....na haina haja ya kutumia maneno magumu waelewesheni wananchi kwamba lishe siyo lazima iwe mayai, nyama na samaki wambieni  lishe ni mboga za majani kama matembele, kunde, maharage vyote hivyo ni lishe" amesisitiza Mhe.Malima.

Aidha, ameongeza kuwa  mikataba hiyo inashuka mwanzo ilikuwa kati ya  Mhe.Rais  Samia Suluhu Hassan na Wakuu wa Mikoa na sasa ni Mkuu wa Mkoa na Wahe. Wakuu wa Wilaya na baadaye Wakurugenzi.

Hata hivyo, Mhe.Malima ameongeza kuwa Jambo kubwa katika mikataba ya Lishe ni Elimu juu ya Swala la lishe, kwa kuwa vitu vyote vinavyohusu Lishe vinapatikana katika mazingira ya wananchi.

"Wapeni  Elimu wananchi  juu ya matumizi ya vyakula hivyo ili viwaletee afya watoto wetu,"amesisitiza

Naye, Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt.Thomas Rutachunzibwa amesema mkataba huu ni wa msingi sana ukizingatia kuwa hali ya Udumavu iko juu takriban asilimia 29 katika mkoa wa Mwanza hivyo wameupokea Mkataba huo na kuahidi kuusimamia katika utekelezaji wake.

Kwa upande wake Bw.Daniel Machunda Katibu Tawala Msaidizi Utawala  Mkoa wa Mwanza  akimuwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa huo Balandya Elikana, awali akimkaribisha Mhe.Mkuu wa Mkoa amesema kikao hicho ni kufuatia agizo la Mhe.Rais  Samia Suluhu Hassan kuwa ifikapo Oktoba 30 Mikataba yote ya Lishe iwe imesainiwa.

Kikao hiki kimefanyika kufuatia maelekezo ya kikao kazi yaliyotolewa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, na Maafisa Lishe walio katika Sekretarieti za Mkoa kilichofanyika Mwezi Septemba, 2022 Mkoani Dodoma kuhusu Afua za Lishe, ambapo Mhe.Rais alielekeza Ofisi ya Rais TAMISEMI Kupitia Ofisi za Wakuu wa Mikoa na Wilaya kusaini mikataba ya Utendaji kuhusu masuala ya Lishe kati ya Mkoa na Halmashauri zao zote.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.