• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malima awaasa Wauguzi kuutumia vyema Mkutano wao Mkuu kutatua changamoto zao

Posted on: May 8th, 2023

RC Malima awataka Wauguzi kuutumia Mkutano wao Mkuu kutatua changamoto zao


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Adam Malima amewataka Wauguzi wanaoshiriki Mkutano wao Mkuu wa Chama cha Wauguzi nchini,TANNA unaofanyika Mkoani humo kuutumia kikamilifu kutatua changamoto zao ili kuboresha mazingira yao ya kazi.

Alifungua leo Mkutano huo wa 50 wa Chama hicho kwenye ukumbi wa Malaika Resort uliopo Jijini Mwanza,Mkuu huyo wa Mkoa amesema Wauguzi ni nguzo muhimu kwenye Sekta ya afya licha ya kukabiliwa na mazingira magumu na hatarishi katika kazi zao,hivyo Mkutano huo ndiyo jukwaa la kupaza sauti ili kasoro zilipo zifanyiwe kazi.

"Mmefanya uamuzi wa busara kuuleta Mkutano huu wa Kitaifa Mkoani Mwanza,niwasihi sana msikae hapa kwa siku tano na kuuchukulia kirahisi tu bali hakikisheni unakuja  mageuzi chanya ili kuendelea kufanya kazi katika mazingira bora na salama",Amesisitiza Mhe.Malima.

Amesema Serikali ya awamu ya sita imezidi kuimarisha Sekta hiyo kwa kuhakikisha kunakuwepo na Hospitali na vituo vya afya vyenye ubora pamoja na upatikanaji wa dawa kwa wakati na hivi karibuni imetoa ajira 8070 kada ya afya.

"Mkutano huu tunaimani utakuja na matokeo chanya hasa kutokana na fursa za kuelimishana kupitia tafiti za kisayansi zilizofanyika,majadiliano na namna ya kuzitatua changamoto zinazotukabili yote ni baadhi ya faida kupitia Mkutano huu wa Kitaifa",Julius Shigella,Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza.

Kwa upande wake Rais wa Chama cha Wauguzi nchini,Alexander Baluya amesema Mkutano huo umebeba mambo makuu matatu,Kongamano la Kisayansi lililoanza leo na kesho,Mkutano Mkuu wa 50 na siku ya Wauguzi Duniani inayoadhimishwa kila Mei 12 ambayo wataiadhimisha siku ya kufunga Mkutano huo.

"Mkoa wa Mwanza tuna jumla ya Wauguzi 4000 na vituo vya afya 600,licha ya uchache wetu na kuhudumia idadi kubwa ya wateja,lakini Wauguzi tumesimama imara kuhakikisha tunatoa huduma bora siku zote",Claudia Kaluli,Muuguzi Mkuu Mkoa wa Mwanza.

Mkutano huo uliobeba kauli mbiu ya WAUGUZI WETU,MUSTAKBARI WETU umewajumuisha washiriki 1200 wakiwemo Wauguzi wakuu kuanzia ngazi ya Mikoa na Wilaya.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.