• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malima awahakikishia wananchi Sengerema ulinzi na usalama miradi ya Barabara na Kivuko

Posted on: April 23rd, 2023


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mh.Adam Malima amemshukuru Rais Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuonesha kwa vitendo Miradi ya kuwainua wananchi kiuchumi na kuwaahidi wakazi wa Sengerema ulinzi na usalama wa Miradi iliyosainiwa leo ya Barabara ya Sengerema-Nyehunge ya KM 54.4 na Kivuko cha Buyagu-Mbalika.

Akimkaribisha Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi,Mhe.Mhandisi Godfrey Kasekenya kwenye hafla ya utiaji saini wa Miradi hiyo kwenye viwanja vya mnadani Wilayani Sengerema,Mhe.Malima amesema hayupo tayari kushuhudia uhujumu uchumi kwenye Miradi hiyo kwa kufanyika udokozi wa aina yoyote wakati Serikali ya Rais Samia ikiwa mstari wa mbele kuwapigania maendeleo wananchi wake.

"Leo tumeshuhudia muendelezo wa miradi mingi hapa Mkoani kwetu,huu wa Barabara umegharimu zaidi ya Shs Bilioni 73 na wa Kivuko zaidi ya Shs Bilioni 3 ni lazima tuoneshe umakini kwenye Miradi hii yenye tija kwa wananchi".Amesisitiza Mkuu huyo wa Mkoa

Aidha amewakumbusha Wakandarasi walioshinda zabuni hizo kuwa na weledi katika kazi zao ziwe na ubora na  kukamalisha kwa wakati miradi hiyo ili kuharakisha maendeleo ya wananchi.

"Nawapongeza sana Wabunge wa Mkoa wa Mwanza,Mhe.Eric Shigongo wa Buchosa,Mhe.Alexander Mnyeti wa Misungwi na Mhe.Hamis Tabasamu wa Sengerema mnafanya kazi kubwa ya kuwapigania maendeleo wananchi wenu hali ambayo nami mnanirahisishia   kwa kiwango kikubwa,asanteni sana".Mhe.Malima.


"Kwa mwaka huu tuna jumla ya Vivuko vipya 6 vilivyo gharimu Sh Bilioni 33.2 na vya ukarabati vipo 18 vilivyogharimu Shs Bilioni27.5,hii inaonesha ni jinsi gani Serikali ya awamu ya Sita ilivyoweka kipaumbele uimarishaji wa miundombinu ambayo ni nguzo muhimu wa uchumi wa nchi"Mhe.Mhandisi Godfrey Kasekenya,Naibu Waziri  wa Ujenzi na Uchukuzi.

Akizungumzia ujenzi wa barabara hiyo Mbunge wa Sengerema Mhe.Hamis Tabasamu amesema kwa muda mrefu shughuli za kiuchumi kuanzia za mazao ya Uvuvi na kilimo zilizorota kutokana na hali mbaya ya miundombinu ya barabara,lakini kwa ujenzi huo sasa utakuwa na tija pia kwa Halmashauri za Sengerema na Buchosa.

"Mheshimiwa Naibu Waziri Kasekenya nakupongeza kwa hatua hii,lakini jimboni kwangu barabara ya Mwanangwa-Misasi hadi Kahama mwaka huu usiponiwekea kiwango cha lami sitakuelewa nimeizungumzia kwa muda mrefu sana kutokana na umuhimu wake."Mhe Alexander Mnyeti Mbunge wa Misungwi.

"Binafsi namshukuru sana Mhe.Rais Jimbo langu asilimia kubwa wakazi wake wapo visiwani,kuimarishiwa barabara hii ni ukombozi kwao hasa katika shughuli zao za Uvuvi kwani watakuwa wanafanya kazi zao kwa uhakika".Mhe.Eric Shigongo,Mbunge wa Buchosa.

Utiaji huo wa saini kwa upande wa barabara umewahusisha Mtendaji Mkuu wa Tanroad nchini Mhandisi Rogatus Mativila na Mkandarasi AVM Construction kutoka Uturuki na upande w Kivuko alikuwa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa ufundi na umeme TEMESA, Mhandisi Lazaro Kilahala na Mkandarasi Songoro Marine.

Kwa mujibu wa mikataba hiyo Ujenzi wa barabara utachukua muda wa miaka miwili na miezi minne na Kivuko ni miezi kumi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.