• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malima awahimiza Vijana umuhimu wa kujiajiri

Posted on: August 18th, 2022


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Adam Malima amekabidhi Vifaa vyenye thamani ya zaidi ya Milioni 104 kwa Vikundi vya vijana wajasiriamali 168 vilivyotolewa na Shirika la Plan International baada ya kuhitimu na kufuzu mafunzo katika fani mbalimbali tayari kwenda kujitafutia kipato.

Akizungumza na vijana hao waliohitimu mafunzo chini ya mradi wa 'Vijana, Maisha na Kazi' katika hafla ya Kukabidhi vifaa iliyofanyika leo Agosti 18, 2022 kwenye viwanja vya Chuo cha Ufundi Stadi (VETA) Mwanza, Mhe. Malima ametoa wito kwa wahitimu kuyatumia mafunzo hayo kwa weledi na bidii kubwa katika kujitafutia ridhki kwa ustawi wa familia zao.

"Hakuna malipo ya wema kama si kufanya wema wenyewe, mradi huu wema wake ni kwamba umetoa Elimu na Ujuzi ambao vijana hawa wamepata na hakuna mtu anaweza kuwanyang'anya hata kama mtu akipoteza Cheti za ujuzi huo, tunawashukuru sana wadau wetu." Mhe. Malima.

Vilevile, Mkuu wa mkoa amekemea tabia ya kunyanyapaa watu wenye ulemavu huku akibainisha kuwa kuzaliwa na ulemavu sio laana bali ni majaaliwa ya mwenyezi Mungu na wanapaswa kupata nafasi kwenye kila kitu kama ambavyo wadau wa mafunzo hao walivyowapatia fursa ya kupata Ujuzi na Vifaa hivyo.

Mkuu wa Wilaya ya Ilemela, Mhe. Hassan Masala ametoa pongeza kwa Shirika la Plan International, VETA na Wadau wengine wanaosaidia Serikali katika juhudi za kusaidia kutimiza malengo ya maendeleo kwa wananchi wake.

Mkurugenzi wa VETA kanda ya Ziwa Charles Kangele amewashukuru shirika la Plan International na ametumia wasaa huo kuwakaribisha wananchi kupata ujuzi na mafunzo stadi kwenye fani 11 zinazotolewa na Chuo cha VETA Mwanza na akabainisha kuwa Wilaya za Kwimba na Ukerewe wako mbioni kupata Vyuo vipya.

Meneja wa Shirika la Plan International wa Mikoa ya Mwanza na Mara Bwana Rwambali Majani amesema vijana 168 wamefuzu mafunzo kwa kushirikiana na VETA na wadau wengine katika fani za Ushonaji, Uchomeleaji, Ufundi Magari, Umeme wa Magari, Kutengeneza bidhaa za Almanium na Mabomba.

"Tunakabidhi vifaa vyenye thamani ya zaidi ya Milioni 104 ambavyo vitawasaidia katika kuzalisha kwa ustawi wa maisha yao wenyewe na ujenzi wa Taifa kwa Ujumla na mradi huu unafanya kazi kwenye kata 11 na kwa kushirikiana na SIDO, TAHA, VETA na SEDIT na tumewawezesha kwa gharama za mafunzo, usafiri na gharama za kulea watoto kwa waliojifungua wakiwa kwenye mafunzo." Amesema Majani.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.