• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malima awashauri Makatibu Tawala Wasaidizi Mipango na Uratibu kuwa na weledi katika kusimamia miradi

Posted on: November 8th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Adam Malima amewakumbusha Makatibu Tawala Wasaidizi Mipango na Uratibu kutanguliza Weledi katika majukumu yao ili miradi ya maendeleo wanayoisimamia iwe na tija kwa Taifa.

Akifungua leo mafunzo ya siku tatu kwa viongozi hao kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa yenye lengo la kuwaelimisha namna ya kuandika na kusimamia miradi,Mhe Malima amesema viongozi hao ndiyo uti wa mgongo kwenye Ofisi za Mikoa kutokana na jukumu lao linalogusa maendeleo ya wananchi.

"Rai yangu kwenu zingatieni sana mafunzo haya huko mlikotoka natambua mna miradi mingi kuanzia Sekta ya afya na miundombinu,mkirudi muoneshe mageuzi chanya" amesema Mkuu huyo wa Mkoa.

Mhe Malima amebainisha Serikali ya awamu ya Sita imesambaza miradi mingi ikiwemo ya kimkakati kila kona ya nchi hii hivyo viongozi hao watambue mchango wao wa kuhakikisha ina ubora na kukamilika kwa wakati.

"Nami ni mchumi kama nyie hakuna nisichofahamu epukeni kutanguliza tamaa na kuhujumu miradi mnayosimamia na pia kuwa na kauli za kilaghai ili kuwafurahisha Viongozi wenu,mkifanya hivyo mtarudisha nyuma ndoto za wananchi za kupata maendeleo" amesisitiza Mhe.Malima

Awali akimkaribisha mgeni rasmi,Mkurugenzi msaidizi Idara ya Tawala za Mikoa kutoka TAMISEMI,Johnson Nyingi amesema mafunzo hayo yamewajumuisha Makatibu Tawala Wasaidizi kutoka Mikoa 25,wakiwezeshwa na Wataalamu wa masuala ya Uchumi kutoka Chuo Kikuu cha Mzumbe.

Mafunzo hayo yanafanyika  Mwanza,.Mkoa ambao una Miradi mikubwa ya kimkakati yakiwemo Masoko,Stendi za mabasi,Reli ya Kisasa SGR, ujenzi wa Meli mpya ya Mv Mwanza pamoja na Daraja la JP Magufuli.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.