• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malima awakumbusha Madiwani kusimamia na kuendeleza vyema rasilimali za Bonde la Ziwa Victoria

Posted on: March 31st, 2023


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Adam Malima amewataka Halmashauri wanachama wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Kanda ya Ziwa Victoria, LVRLAC kusimamia na kuendeleza rasilimali za Ziwa Victoria ili ziendelee kuwa na tija kwa wananchi kutoka nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Mhe. Malima akizungumza leo wakati wa kufungua mkutano mkuu wa 27 wa Taasisi hiyo Jijini Mwanza amesema Madiwani wana wajibu mkubwa wa kuhakikisha wanaweka mikakati ya kisasa ukiwemo muda wa uvuaji wa samaki bila kuhofia nafasi zao za kisiasa kwa lengo la kuzidi kulifanya ziwa hilo kuwa nguzo muhimu ya  uchumi.

"Ndugu zangu Madiwani nyie lazima matumbue mna changamoto kubwa ya kupaza sauti kwa niaba ya wananchi mnao wawakilisha,tukifanya mambo kwa kuingiza siasa hili Ziwa letu litageuka kuwa jangwa kwa maana ya kutoweka kwa rasilimali zilizomo ziwani humo".Amehimiza Mkuu huyo wa Mkoa.

Amesema Serikali sasa imetoa fedha nyingi kwenye Sekta ya Uvuvi na Kilimo waitumie fursa ya asilimia kumi inayotengwa na Halmashauri kuwawekea mazingira mazuri ya kujiajiri vikundi vya Vijana kwa kujikita kwenye kilimo cha umwagiliaji na ufugaji wa samaki kwa kutumia vizimba pamoja na Utalii.

"Ziwa letu lina visiwa vingi sana kama vile Ilugwa,Gana na Mbinguni huko kuna vivutio vingi ambavyo tukivitumia vizuri vitaleta watalii wengi na kuinua uchumi wa mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla"RC Malima.

Aidha ameshauri mikutano ijayo ya Taasisi hiyo wawajumuishe Taasisi za Kimataifa zinazojihusisha na masuala ya mazingira,Wakuu wa Mikoa,na Wakuu wa Wilaya ili agenda zao zibebe uzito na kufanyiwa kazi kikamilifu.

Akimkaribisha mgeni rasmi kufungua mkutano huo Mwenyekiti wa Taifa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Kanda ya Ziwa Victoria LVRLAC,William Gumbo amesema Taasisi hiyo yenye jumla ya Halmashauri 130 kutoka Tanzania na nchi wanachama Kenya na Uganda imeweza kupiga hatua katika majukumu yake ya kutunza mazingira ikiwemo kupanda miti na utunzaji wa ziwa Vitoria.

"Mhe mgeni rasmi miongoni mwa majukumu yetu kuyalinda mazingira ili yawe endevu kwa vizazi vijavyo pamoja na ziwa Victoria,nikiri bado tunahitaji nguvu ya pamoja katika kutimiza majukumu haya hasa upande wa ziwa bado zipo changamoto nyingi ikiwemo utumiaji usiyo sahihi wa ziwa Victoria kama kutupa taka ngumu,uvuaji haramu wa samaki yote haya yanahitaji uwajibikaji wa kweli ili kutimiza malengo tuliyoyakusudia."William Gumbo M/kiti LVRLAC Taifa.

Mkutano huo umejumuisha Halmashauri 47 kutoka Mikoa sita ya Geita,Shinyanga,Simiyu,Mwanza,Mara na Kagera huku Kauli mbiu yake ikisema Juhudi endelevu kati ya Tawala za Mitaa na Jamii katika kudhibiti mabadiliko ya Tabia nchi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.