• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malima aziagiza Halmashauri Mkoani Mwanza kutenga fedha za Lishe

Posted on: September 21st, 2022


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima amewataka watekelezaji wa Mkataba wa Lishe Mkoani humo kutilia Mkazo Afua za Lishe ikiwa ni pamoja na kutenga fedha na suala hilo kuwa ajenda ya kudumu kwenye vikao ili kuondoa tatizo la Udumavu na utapiamlo kwa watoto.

Mhe. Malima amebainishwa hayo leo Septemba 21, 2022 wakati wa Mkutano wa tathmini ya Mkataba wa Lishe ulioangazia Afua za kufanikisha huku akibainisha kuwa Ukamilishaji wa miradi ya Maji kwa wakati na Mkazo wa Elimu kwa watoto kuwa ni miongoni nyenzo za kufanikisha lishe bora.

"Kila tunapokaa kwenye vikao vyetu tuweke ajenda ya lishe ili watu watambue nini kinaendelea na mambo yanayosababisha lishe duni ni pamoja na Matunzo duni ya mama na mtoto, tamaduni zisizofaa kama nyama kula baba pekee na ulaji usiofaa wa vyakula hivyo lazima tuepukane nayo na tuongeze uelewa wa umuhimu wa lishe kwa jamii." Amesema Malima.

"Mhe. Mkuu wa Mkoa, Viashiria vinaonesha tunakwenda vizuri kilichobaki ni wadau wote kuendelea kushirikiana katika kutekeleza shughuli za mkataba wa lishe ili kujenga pia jamii yenye afya njema." Amesema Katibu Tawala wa Mkoa, Balandya Elikana.

Mkuu wa Wilaya ya Magu, Mhe. Salum Kalli amesisitiza kuwa kwa kuzingatia Mkoa umekua ukifanya vizuri kwenye masuala mbalimbali kama Chanjo ya Uviko 19 ambapo Wilaya ya Ukerewe imekua Kinara, basi wataalamu wanapaswa kusimama imara kwenye kila kitu kama Ukusanyaji wa mapato ili uboreshaji wa Miundombinu ya Afya uende sambamba na uboreshaji wa afua za Lishe.

"Twendeni tukazingatie sana masuala haya ili tunapowasilisha taarifa za masuala ya Lishe kwenye ngazi ya Taifa Mkoa wa Mwanza kwa umuhimu wake tuwe wa kwanza kwenye utekelezaji wa Afua za lishe katika kuzingatia jamii inaimarika" Mhe. Kalli.

"Kwa mwaka huu kuna unafuu mkubwa kwenye kipengele cha fedha kwani Halmashauri zimepelekeka fedha kwa zaidi ya asilimia 70 ya fedha zinazohitajika kwenye afua za Lishe tofauti na asilimia 50 pekee ya fedha zilizopelekwa mwaka uliopita, lakini vilevile bado tuna changamoto ya upelekeji wa chakula chenye virutubisho kwenye shule." Amesema Dkt. Thomas Rutachunzibwa, Mganga Mkuu wa Mkoa.

Akichangia mada ya Magonjwa mlipuko, Mganga Mkuu ametoa wito kwa Halmashauri kuandaa maeneo ambayo yatapokea wagonjwa wa Ebola endapo watatokea na waisisitize jamii kuchukua tahadhari zinazotolewa na wataalamu wa Afya katika kujikinga dhidi ya ugonjwa huo ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa mara moja atakapotokea mgonjwa.

Naye, Mratibu Huduma za Chanjo Mkoa Amos Kiteleja amezitaadharisha Halmashauri kujiandaa na Mlipuko wa Ugonjwa wa Surua kwani kuna viashiria kutokana na kuwa na wagonjwa watano wa tatizo hilo na vilevile ameipongeza Halmashauri ya Buchosa kwa kufikia asilimia 90 ya utoaji chanjo za magonjwa mbalimbali na kufikia lengo la Taifa.

Awali Dkt. Mabai Leonard Mratibu Huduma za Matibabu ya Magonjwa ya Mlipuko Mkoa amesema kuwa katika kukabiliana na Mlipuko wa Ugonjwa wa Ebola wataalamu wameshaanza kutoa Elimu ya jinsi ya kujikinga na kwamba kimeshaandaliwa kituo maalum cha kutolea huduma hizo endapo atatokea.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.