• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malima kesho awaalika wananchi na wale kutoka Mikoa jirani kuja kushuhudia kuingizwa Ziwani Viktoria Meli ya Mv Mwanza HAPA KAZI TU

Posted on: February 11th, 2023


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Adam Malima amewakaribisha Wananchi wote na wale kutoka Mikoa jirani kuja Kwa wingi siku ya kesho kushuhudia Meli ya Mv Mwanza HAPA KAZI TU kutolewa kwenye chelezo na kuingizwa Ziwani Viktoria.

Akizungumza leo na Vyombo vya habari kwenye  Ukumbi mkubwa wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa,Mhe.Malima amesema hii ni hatua ya pili kubwa katika ukamilishaji wa ujenzi wa Meli hiyo ambayo ni historia kwenye vyombo vya usafiri wa majini kwenye maziwa makuu hapa nchini.

"Tuna kila sababu ya kuishukuru Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Dkt.Samia Suluhu Hassan ambaye ameendelea kukuza Uchumi wa Taifa letu kwa vitendo hivyo Wananchi tuna kila sababu ya kuja kuyashuhudia matokeo chanya ya Miradi hii ya kimkakati".Amesema Mkuu wa Mkoa.

Mhe.Malima amebainisha baada ya chombo hicho kuingizwa majini, mwezi Juni mwaka huu litafuata tukio la Meli hiyo kuanza kutoa huduma.

"Hili ni tukio muhimu na la kihistoria kwenye nchi yetu na ukanda wa Afrika wenye Maziwa  ambapo hii ndiyo Meli kubwa kuliko zote,uzito wa tano 3500, urefu wa mita 92.6, na Upanga wa mita 17,  tujivunie mradi huu mkubwa"Eric Hamiss Mkurugenzi wa Kampuni ya Huduma za Meli.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni ya Huduma za Meli Meja Jenerali mstaafu John Mbungo amesema hili ni tukio kubwa na kihistoria kwa nchi za Afrika Mashariki ni uwekezaji wenye tija ambao wananchi wana kila sababu ya kuishukuru Serikali ya Dkt.Samia.

Meli ya Mv Mwanza HAPA KAZI TU ilianza kujengwa Januari 2019 na Kampuni ya GAS Entec Limited kwa kushirikiana na Suma JKT kwa gharama ya Shs Bilioni 109.15.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.