• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malima kuweka shamba la Pamba la mfano Sengerema

Posted on: March 2nd, 2023


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima amepania kuinua zao la Pamba lenye ubora kwa kuweka shamba la mfano kata ya Buyagu Wilayani Sengerema.

Akizungumza na baadhi ya wakulima alipotembelea mashamba yao ya Pamba, Mhe. Malima amesema bado wakulima wa zao hilo hawatumii kilimo cha kisasa, sasa ameamua kuwasilisha mpango wa kuweka kilimo cha kisasa Bodi ya Taifa ya Pamba baada ya kupata hekari za kutosha kwa kuwatumia wakulima ambao watakuwa tayari kuingia katika mpango huo.

"Mimi ni Mwenyekiti wa kamati ndogo ya Uzalishaji wa zao la Pamba kwenye bodi ya Taifa, nitatumia fursa ya kikao chetu kijacho huko Mkoani Simiyu kuuzungumzia mpango huu lengo ni miaka michache ijayo mkulima avune tani milioni moja." Malima amesisitiza.

Amebainisha kuwa mpango huo utahusisha kuwaleta wakulima Wataalamu watakaopima udongo, kutoa ushauri aina ya mbolea husika na namna ya upandaji kwa kuzingatia kanuni bora za kilimo ili mkulima kila hekari moja apate kilo 2000.

Ameongeza kuwa mara baada ya kuyakagua mashamba hayo amesikitishwa kutokana na kuwaona wakulima wakipoteza fursa ya kupata fedha nyingi kama wangetumia ulimaji wa kisasa unaohimizwa.

"Hapa nimelima kwa kutumia utaratibu wa kienyeji tu sijatumia utaalamu wowote wala kuweka mbolea, hii imetokana na kutofikiwa na Wataalamu nikaamua nilime tu nilivyozoea." Maneno Maneno, Mkulima wa Pamba.

Mkoa wa Mwanza unalima Pamba Wilaya 4 za Sengerema,Kwimba,Misungwi, na Magu na mwaka jana imevuna Pamba kilo milioni 16.

Aidha Mhe. Malima akiwa njiani kwenda Mgodi wa Nyanzaga kupata taarifa za maendeleo ya fidia za wakazi jirani na eneo hilo, amesimama kata ya Igarula katika mkutano wa hadhara na wananchi na kuwahakikishia mradi wa maji wa Shs Bilioni 13.7 unaotekelezwa na SEWASA kuwa utakamilika kwa wakati.

Kuhusu changamoto ya uchache wa Bweni Shule ya Sekondari ya Ngoma, Mhe.Malima ameahidi kuongeza mabweni mawili la wasichana na wavulana ili kuwapunguzia adha ya kutembea umbali mrefu wanafunzi hao.

"Niwasihi sana wananchi muwe na utulivu na msikubali kudanganywa na wachache watakaokuja kwa nia ya kuchochea migogoro wakati mkiwa mbioni kulipwa fidia na Mgodi wa Nyanzaga". Amesisitiza Mkuu huyo wa Mkoa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.