• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Mongella achukua hatua kwa waliohusika wizi wa mitihani

Posted on: October 6th, 2018


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongella amewataka Wakurugenzi watendaji wa  Jiji la Mwanza, Kwimba na Buchosa kuchukua maamuzi ya mapendekezo yaliyotolewa na Baraza la Mitihani la Taifa(NECTA) na Naibu Katibu Mkuu wa Elimu Tamisemi waliyoyatoa wakati wanatangaza kufuta matokeo ya darasa la saba kwa shule zilizohusika na wizi wa mitihani    zikiwemo tatu za jiji la Mwanza.

Mhe. Mongella amesema wamiliki wa shule, wakuu wa shule na baadhi ya walimu ndiyo wahusika wakuu wa kuiba mitihani wakiwa na lengo la kufaurisha watoto wengi ili wazazi waamini shule husika na kupeleka watoto wengi zaidi katika shule hizo.

“Ninawasiwasi hata kwenye idara zetu za elimu kuna watu wanahusika, ninachokitegemea wote walioelekezwa kuondolewa kwenye nafasi zao wakisubiri mamlaka zao kufanya  maamuzi kufikia leo saa sita ,maamuzi yawe yamechukuliwa  sitegemei mkurugenzi wa kwimba, jiji la mwanza na Buchosa kutofanya maamuzi, tutamfanyia yeye maamuzi,”alisema Mongella.

Aliwataka wamiliki na wakuu wa shule wenye tabia ya kuiba mitihani waache kwa kuwa watachukuliwa hatua kali za kisheria ikiwemo kuvuliwa wadhifa wao na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Dkt.Philis Nyimbi alisema waliokamatwa kwa kuiba mitihani inaonekana walianza muda mrefu kwa kuwa za mwizi ni 40 ndio maana wamekamatwa.

“Tumesikitishwa sana Wilaya yetu kutiwa doa la wizi wa mitihani na baadhi ya watu wachache wasio waadilifu licha ya wilaya kujitahidi kufanya mambo ya kuleta maendeleo,”alisema Dkt. Nyimbi.

Hata hivyo Mhe.Mongella amewaagiza Takukuru na polisi kuchukua hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kukamatwa wakati wakisubiri Mamlaka zao kufanya maamuzi.

"Kufikia leo saa sita kama kuna mtu amefanya  uzembe wa kutochukua maamuzi,atafanyiwa yeye maamuzi, nawahitaji walioguswa na hilo, REO nataka nione barua zote za maamuzi hayo,"alisema Mhe. Mongella.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.