• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Mongella awaagiza ma DC kudhibiti mimba mashuleni

Posted on: October 16th, 2018


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongella amewataka viongozi wa Serikali mkoani  Mwanza kuiga mfano wa Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Mhe. Juma Sweda wa kuhakikisha wanawadhibiti watu wanaowapa ujauzito wanafunzi  wa kike na hivyo kukatisha ndoto za maisha kwa kushindwa kuhitimu elimu yao.

Alimpongeza Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Mhe. Juma Sweda na Kamati yake ya ulinzi na usalama kwa hatua ambazo wamechukua za kuwakamata na kuwafikisha mahakamani watu waliobainika kuwapa ujauzito watoto wa kike, akiwemo Mwalimu Peter Fred wa Shule ya Msingi Kifune wilayani humo ambaye amehukumiwa kifungo cha miaka 30 kwenda jela baada ya kubainika kuwa na hatia ya kumpatia ujauzito mwanafunzi.

“Nilipomuona Mwalimu yule kupitia kwenye mitandao na Televisheni  akiwa amepigwa pingu nilifurahi sana, ningekuwa na fedha ningemtumia DC wa Misungwi kwa kweli amefanya kazi kubwa sana," alisema  Mhe. Mongella na kuwataka wakuu wengine wa wilaya kuiga mambo mazuri yanayofanywa na uongozi wa wilaya ya Misungwi katika kudhibiti mimba mashuleni.

Aidha aliwataka wakuu wa wilaya za Ukerewe na Kwimba kuhakikisha wanadhibiti mimba mashuleni, pamoja na wilaya nyingine ili kuboresha elimu kwa mtoto wa kike.

“Kwimba hali ya utiaji wa mimba inatisha, utafikiri wilaya ina mpango maalum wa utiaji mimba kwa wanafunzi na DC mwanamke upo," alisema Mhe. Mongella.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Magu Mhe. Dkt. Philemoni Sengati alikiri kulishughulikia suala la mimba katika wilaya yake, lakini juhudi hizo zimekuwa zinakwamishwa na baadhi ya watendaji wa mahakama kushindwa kutoa haki kwa watuhumiwa wanaokuwa wamebainika kuwapatia ujauzito watoto wa kike.



Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.