• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AAGIZA HATUA KALI DHIDI YA MTUMISHI ALIYEJIPA TENDA MRADI WA HOSPITALI YA RUFAA UKEREWE

Posted on: February 9th, 2026

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda, ameagiza kuchukuliwa hatua za haraka za kinidhamu na kisheria dhidi ya mtumishi wa umma aliyedaiwa kujihusisha na mgongano wa maslahi, wizi wa mali za Serikali na ucheleweshaji wa utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Mkoa yenye hadhi ya Rufaa unaotekelezwa Wilaya ya Ukerewe.

Akizungumza wakati wa ukaguzi wa mradi huo, Mhe. Mtanda amesema changamoto ilianza pale ambapo kampuni ya Nosa, inayomilikiwa na mtumishi wa Serikali, ilipewa tenda ya kusambaza kokoto kwa ajili ya mradi huo, bila mhusika kutangaza maslahi yake (declare interest), jambo ambalo ni kinyume na sheria na maadili ya utumishi wa umma.

Mhe. Mtanda amesema mtumishi huyo alilipwa fedha za Serikali kupitia akaunti yake binafsi, lakini ameshindwa kusambaza kokoto kwa wakati, hali iliyosababisha ucheleweshaji wa mradi na kumkwamisha mkandarasi.

“Haya hatuwezi kuyakubali. Mtumishi wa Serikali kujipa tenda, asitangaze maslahi, alipwe kwenye akaunti binafsi halafu achelewesha mradi wa wananchi hili ni kosa kubwa,” amesema Mhe. Mtanda.

Ameeleza pia kuwa nondo zenye thamani ya shilingi milioni 9 ziliibwa na kuuzwa kwa shilingi milioni 2 kwa mtumishi huyo, huku aliyefanikisha uuzaji huo akiwa ni mtumishi wa Halmashauri. Amelipongeza Jeshi la Polisi kwa hatua ya kuwakamata watuhumiwa wa tukio hilo.

Kutokana na hilo, Mkuu wa Mkoa amemuagiza Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza (RAS) kuhakikisha mtumishi huyo anachukuliwa hatua za kinidhamu mara moja, huku Jeshi la Polisi (NPS) likitakiwa kufungua kesi ya jinai na kumfikisha mtuhumiwa mahakamani Mwanza.

“Huyu mtumishi hatakiwi kulindwa hapa Ukerewe. Hii ni kesi ya wizi. NPS andikeni kesi inayomfaa na ahukumiwe kwa mujibu wa sheria. Tusipofanya hivyo, mradi huu utachelewa kukamilika,” amesisitiza.

Mhe. Mtanda amesema kucheleweshwa kwa mradi huo kutawafanya wananchi kuichukia Serikali, licha ya Serikali Kuu kutoa zaidi ya shilingi bilioni 26 kwa ajili ya ujenzi wa hospitali hiyo, akionya kuwa watu wachache hawapaswi kuhujumu juhudi za Serikali za kuboresha huduma za afya.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI IDARA YA MAAFA OWM AFUNGA MAFUNZO YA KUKABILIANA NA DHARULA MWANZA

    February 20, 2026
  • KAYA 19,344 KUNUFAIKA NA BIMA YA AFYA KWA WOTE MWANZA AWAMU YA KWANZA

    February 20, 2026
  • RC MTANDA AMPOKEA WAZIRI DEUS SANGU MWANZA

    February 20, 2026
  • RC MTANDA AWATAKA WASIMBE NA WABANZA KUUNGANA KUKATA BIMA YA AFYA KWA WOTE

    February 20, 2026
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.