• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AAGIZA KUIMARISHWA HUDUMA ZA MAABARA ZAHANATI YA NYAMBITI, ILEMELA

Posted on: February 10th, 2026

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ametoa agizo kwa Mganga Mkuu wa Mkoa kuhakikisha Zahanati ya Nyambiti iliyopo Mtaa wa Nyambiti, katika Manispaa ya Ilemela inapatiwa Mtaalamu wa Maabara pamoja na vifaa muhimu ili kuwasaidia wananchi kupata huduma za uchunguzi wa afya karibu na makazi yao.

Mhe. Mtanda ametoa agizo hilo wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua ujenzi wa Zahanati ya Nyambiti Kata ya Buzuruga, ambapo amesema kuwa hakuna sababu ya wananchi kusafiri umbali mrefu kwenda Hospitali za Rufaa, Mkoa au Wilaya ilhali huduma hizo zinaweza kutolewa katika zahanati hiyo.

Amesisitiza kuwa lengo la Serikali ni kusogeza huduma za afya karibu na wananchi ili kupunguza msongamano katika hospitali kubwa na kuhakikisha matatizo madogo ya kiafya yanatatuliwa katika ngazi ya chini.

“Tunajenga zahanati na vituo vya afya ili matatizo madogo madogo yamalizwe huko huko, badala ya kulundikana katika hospitali kubwa,” amesema Mhe. Mtanda.

Mkuu wa Mkoa amewahakikishia wananchi wa Nyambiti kuwa vifaa vya maabara vitapatikana baada ya maagizo aliyoyatoa kwa Mganga Mkuu wa Mkoa, huku akiahidi kufuatilia utekelezaji wa agizo hilo ndani ya kipindi cha miezi miwili.

Aidha, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuidhinisha kiasi cha shilingi milioni 239 kupitia Sekta ya Afya kwa mwaka wa fedha 2024/2025, ambapo sehemu ya fedha hizo imetumika katika ujenzi wa Zahanati ya Nyambiti.

Katika hatua nyingine, Mhe. Mtanda amemuelekeza Mganga Mkuu wa Wilaya ya Ilemela kuhakikisha mfumo wa GOTHOMIS unafungwa ipasavyo ili kuwezesha baadhi ya changamoto za uendeshaji wa kituo hicho kutatuliwa kupitia mapato ya ndani.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI IDARA YA MAAFA OWM AFUNGA MAFUNZO YA KUKABILIANA NA DHARULA MWANZA

    February 20, 2026
  • KAYA 19,344 KUNUFAIKA NA BIMA YA AFYA KWA WOTE MWANZA AWAMU YA KWANZA

    February 20, 2026
  • RC MTANDA AMPOKEA WAZIRI DEUS SANGU MWANZA

    February 20, 2026
  • RC MTANDA AWATAKA WASIMBE NA WABANZA KUUNGANA KUKATA BIMA YA AFYA KWA WOTE

    February 20, 2026
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.