• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AAHIDI USIMAMIZI MZURI WA KODI, ELIMU NA KUTAKA MALEZI BORA KWA VIJANA

Posted on: April 11th, 2024

RC MTANDA AAHIDI USIMAMIZI MZURI WA KODI, ELIMU NA KUTAKA MALEZI BORA KWA VIJANA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo Aprili 11, 2024 ameshiriki Baraza la Eid El Fetr kama mgeni rasmi na kuahidi usimamizi mzuri wa Kodi bila kuonewa mtu, asisitiza elimu na amewataka wazazi kukumbuka wajibu wao wa malezi bora vijana.

Akizungumza na washiriki wa Baraza hilo kwenye ukumbi wa BoT, Mkuu huyo wa Mkoa amesema hakuna Taifa lolote lililoendelea bila ya kuwa na mpango mzuri wa ulipaji wa kodi hivyo atasimamia kikamilifu na kutanguliza uungwana kwa wafanyabiashara.

"Sipo tayari kuona nguvu ikitumika katika utekelezaji wa sheria za nchi iwe kwa mwananchi yoyote wakiwemo wafanyabiashara, napenda mashauriano zaidi na kuchukua maamuzi," amesema Mtanda.

Kuhusu suala la elimu amesema ni wajibu wa kila mzazi kutimiza haki za watoto wao kwa kuhakikisha wanakwenda shule kikamilifu.

Akizungumza suala la malezi Mtanda amekemea tabia iliyoibuka hivi sasa kwa baadhi ya Wanawake wenye vipato kujigamba wao ni 'SINGLE MOTHER' na kusisitiza malezi bora ni kwa wazazi wote wawili

"Familia yenye malezi bora kwa watoto wao mnaturahisishia hata sisi viongozi kuwaongoza watu wenye weledi wa tabia hivyo Taifa linakuwa na watu waliostaarabika.

Aidha amewakumbusha viongozi wote wa dini kuendelea kuwaombea viongozi wetu wa juu  kuwa na afya njema na hekima ya kuliongoza Taifa letu.

"Rais Samia katuletea miradi mingi ya kimkakati yenye thamani ya ma trioni ya fedha ikiwemo reli ya kisasa SGR,Meli ya Mv Mwanza,Daraja la JP Magufuli na sasa unapanuliwa uwanja wa ndege uwe wa knimataifa,ni wajibu wa kila mmoja kumshukuru na kumuombea",RC Mtanda.

Akimkaribisha mgeni rasmi kwenye Baraza la Eid,Shehe mkuu wa mkoa wa Mwanza,Hassan Kabeke amesema wao kama viongozi wa dini wataendelea kuiunga mkono Serikali katika ujenzi wa Taifa na tayari wana kauli mbiu kwa waumini wao isemayo Shiriki uchaguzi mdogo wa Serikali za mitaa kwa utulivu na amani.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.